Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Chastity

60 mistari · 21 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. baada ya kitambo mke wa Potifa akamtamani Yosefu, akamwambia, “Njoo, ukutane nami kimwili!”

  2. Lakini Yosefu akakataa. Akamwambia yule mwanamke, “Mimi nikiwa katika uongozi, bwana wangu hahusiki na kitu chochote katika nyumba hii, kila kitu alicho nacho amenikabidhi.

  3. Hapa nyumbani hakuna aliye mkuu kuliko mimi. Bwana wangu hakunizuilia kitu chochote isipokuwa wewe, kwa kuwa wewe ni mke wake. Nitawezaje basi kufanya uovu huu na kutenda dhambi dhidi ya Mungu?”

  4. Ingawa yule mwanamke aliendelea kumshawishi Yosefu siku baada ya siku, Yosefu alikataa kukutana naye kimwili wala kukaa karibu naye.

  5. Ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi aliinuka kitandani mwake na kutembeatembea juu ya paa la jumba lake la kifalme. Kutokea kule kwenye paa, akamwona mwanamke akioga. Mwanamke huyo alikuwa mzuri sana wa sura,

  6. naye Daudi akatuma mtu mmoja kuuliza habari za huyo mwanamke. Huyo mtu akamwambia Daudi, “Je, huyu si Bathsheba binti Eliamu, naye ni mke wa Uria, Mhiti?”

  7. Ndipo Daudi akatuma wajumbe kumleta. Huyo mwanamke akaja kwa Daudi, Daudi akakutana naye kimwili. (Huyo mwanamke ndipo tu alikuwa amejitakasa kutoka siku zake za hedhi.) Kisha akarudi nyumbani kwake.

  8. Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.

  9. Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.

  10. Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,

  11. aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.

  12. Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.

  13. Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.

  14. Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.

  15. Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.

  16. Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.

  17. Kunywa maji kutoka kwenye kisima chako mwenyewe, maji yanayotiririka kutoka kwenye kisima chako mwenyewe.

  18. Je, chemchemi zako zifurike katika barabara za mji na vijito vyako vya maji viwanjani?

  19. Na viwe vyako mwenyewe, kamwe visishirikishwe wageni.

  20. Chemchemi yako na ibarikiwe na umfurahie mke wa ujana wako.

  21. Kulungu jike apendaye, kulungu mzuri: matiti yake na yakutosheleze siku zote, nawe utekwe daima na upendo wake.

  22. Kwa nini mwanangu, utekwe na mwanamke kahaba? Kwa nini ukumbatie kifua cha mke wa mwanaume mwingine?

  23. Kwa maana njia za mtu ni wazi kabisa mbele za Bwana, naye huyapima mapito yake yote.

  24. yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.

  25. Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,