Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Mathayo 15:37takriban 32 BK

    Wote wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.

  2. Mathayo 15:38takriban 32 BK

    Idadi ya watu walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.

  3. Mathayo 15:39takriban 32 BK

    Baada ya kuaga ule umati wa watu, Yesu aliingia katika mashua, akaenda sehemu za Magadani.

  4. Mathayo 16:1takriban 32 BK

    Mafarisayo na Masadukayo wakamjia Yesu na kumjaribu kwa kumwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.

  5. Mathayo 16:2takriban 32 BK

    Yesu akawajibu, “Ifikapo jioni, mnasema, ‘Hali ya hewa itakuwa nzuri, kwa kuwa anga ni nyekundu.’

  6. Mathayo 16:3takriban 32 BK

    Nanyi wakati wa asubuhi mnasema, ‘Leo kutakuwa na dhoruba, kwa sababu anga ni nyekundu na mawingu yametanda.’ Mnajua jinsi ya kupambanua kule kuonekana kwa anga, lakini hamwezi kupambanua dalili za nyakati.

  7. Mathayo 16:4takriban 32 BK

    Kizazi kiovu na cha uzinzi kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya Yona.” Yesu akawaacha, akaenda zake.

  8. Mathayo 16:5takriban 32 BK

    Wanafunzi wake walipofika ngʼambo ya bahari, walikuwa wamesahau kuchukua mikate.

  9. Mathayo 16:6takriban 32 BK

    Yesu akawaambia, “Jihadharini. Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na ya Masadukayo.”

  10. Mathayo 16:7takriban 32 BK

    Wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, “Ni kwa sababu hatukuleta mikate.”

  11. Mathayo 16:8takriban 32 BK

    Yesu, akifahamu majadiliano yao, akauliza, “Enyi wa imani haba! Mbona mnajadiliana miongoni mwenu kuhusu kutokuwa na mikate?

  12. Mathayo 16:9takriban 32 BK

    Je, bado hamwelewi? Je, hamkumbuki ile mikate mitano iliyolisha watu 5,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?

  13. Mathayo 16:10takriban 32 BK

    Au ile mikate saba iliyolisha watu 4,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?

  14. Mathayo 16:11takriban 32 BK

    Inakuwaje mnashindwa kuelewa kwamba nilikuwa sisemi nanyi habari za mikate? Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”

  15. Mathayo 16:12takriban 32 BK

    Ndipo wakaelewa kwamba alikuwa hasemi juu ya chachu ya kutengeneza mikate, bali juu ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.

  16. Mathayo 16:13takriban 32 BK

    Basi Yesu alipofika katika eneo la Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake, “Watu husema kwamba mimi Mwana wa Adamu ni nani?”

  17. Mathayo 16:14takriban 32 BK

    Wakamjibu, “Baadhi husema ni Yohana Mbatizaji; wengine husema ni Eliya; na bado wengine husema ni Yeremia au mmojawapo wa manabii.”

  18. Mathayo 16:15takriban 32 BK

    Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?”

  19. Mathayo 16:16takriban 32 BK

    Simoni Petro akamjibu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”

  20. Mathayo 16:17takriban 32 BK

    Naye Yesu akamwambia, “Heri wewe, Simoni Bar-Yona,kwa maana hili halikufunuliwa kwako na mwanadamu, bali na Baba yangu aliye mbinguni.

  21. Mathayo 16:18takriban 32 BK

    Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya Kuzimu hayataweza kulishinda.

  22. Mathayo 16:19takriban 32 BK

    Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni, na lolote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa Mbinguni, nalo lolote utakalofungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.”

  23. Mathayo 16:20takriban 32 BK

    Kisha akawakataza wanafunzi wake wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ndiye Kristo.

  24. Mathayo 16:21takriban 32 BK

    Tangu wakati huo, Yesu alianza kuwaeleza wanafunzi wake kwamba hana budi kwenda Yerusalemu na kupata mateso mengi mikononi mwa wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini siku ya tatu kufufuliwa.

  25. Mathayo 16:22takriban 32 BK

    Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea akisema, “Haiwezekani, Bwana! Jambo hili kamwe halitakupata!”