Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Mathayo 15:12takriban 32 BK

    Kisha wanafunzi wake wakamjia na kumuuliza, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa sana waliposikia yale uliyosema?”

  2. Mathayo 15:13takriban 32 BK

    Akawajibu, “Kila pando ambalo Baba yangu wa mbinguni hakulipanda, litangʼolewa.

  3. Mathayo 15:14takriban 32 BK

    Waacheni; wao ni viongozi vipofu, wanaoongoza vipofu. Kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili watatumbukia shimoni.”

  4. Mathayo 15:15takriban 32 BK

    Petro akasema, “Tueleze maana ya huu mfano.”

  5. Mathayo 15:16takriban 32 BK

    Yesu akawauliza, “Je, bado ninyi hamfahamu?

  6. Mathayo 15:17takriban 32 BK

    Je, hamwelewi kwamba chochote kiingiacho kinywani huenda tumboni, na hatimaye hutolewa nje kikiwa uchafu?

  7. Mathayo 15:18takriban 32 BK

    Lakini kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki ndicho kimtiacho mtu unajisi.

  8. Mathayo 15:19takriban 32 BK

    Kwa maana ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na masingizio.

  9. Mathayo 15:20takriban 32 BK

    Haya ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”

  10. Mathayo 15:21takriban 32 BK

    Yesu aliondoka mahali pale, akaenda sehemu za Tiro na Sidoni.

  11. Mathayo 15:22takriban 32 BK

    Mwanamke mmoja Mkanaani aliyeishi sehemu jirani na hizo akaja kwake akilia, akasema, “Nihurumie, Ee Bwana, Mwana wa Daudi! Binti yangu amepagawa na pepo mchafu, na anateseka sana.”

  12. Mathayo 15:23takriban 32 BK

    Lakini Yesu hakumjibu neno. Hivyo wanafunzi wake wakamwendea na kumsihi sana, wakisema, “Mwambie aende zake, kwa maana anaendelea kutupigia kelele.”

  13. Mathayo 15:24takriban 32 BK

    Yesu akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.”

  14. Mathayo 15:25takriban 32 BK

    Lakini yule mwanamke akaja, akapiga magoti mbele ya Yesu, akasema, “Bwana, nisaidie!”

  15. Mathayo 15:26takriban 32 BK

    Yesu akajibu, “Si haki kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”

  16. Mathayo 15:27takriban 32 BK

    Yule mwanamke akajibu, “Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza za bwana zao.”

  17. Mathayo 15:28takriban 32 BK

    Ndipo Yesu akamwambia, “Mwanamke, imani yako ni kubwa! Iwe kwako kama unavyotaka.” Naye binti yake akapona tangu saa ile.

  18. Mathayo 15:29takriban 32 BK

    Yesu akaondoka na kwenda kando ya Bahari ya Galilaya. Kisha akapanda mlimani, akaketi huko.

  19. Mathayo 15:30takriban 32 BK

    Umati mkubwa wa watu ukamjia, wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; naye akawaponya.

  20. Mathayo 15:31takriban 32 BK

    Hao watu wakashangaa walipoona bubu wakisema, vilema wakipona, viwete wakitembea na vipofu wakiona, wakamtukuza Mungu wa Israeli.

  21. Mathayo 15:32takriban 32 BK

    Kisha Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa muda wa siku tatu, na hawana chakula chochote. Nami sipendi kuwaaga wakiwa na njaa, wasije wakazimia njiani.”

  22. Mathayo 15:33takriban 32 BK

    Wanafunzi wake wakasema, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha umati huu wa watu mkubwa namna hii, nasi tuko nyikani?”

  23. Mathayo 15:34takriban 32 BK

    Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Tunayo mikate saba na visamaki vichache.”

  24. Mathayo 15:35takriban 32 BK

    Yesu akawaambia ule umati wa watu waketi chini.

  25. Mathayo 15:36takriban 32 BK

    Kisha akachukua ile mikate saba na wale samaki, naye akiisha kumshukuru Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake, nao wakawapa ule umati wa watu.