circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Mathayo 13:56takriban 31 BK
Nao dada zake wote, hawako hapa pamoja nasi? Mtu huyu amepata wapi basi mambo haya yote?”
- Mathayo 13:57takriban 31 BK
Wakachukizwa naye. Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani kwake.”
- Mathayo 13:58takriban 31 BK
Naye hakufanya miujiza mingi huko kwa sababu ya kutokuamini kwao.
- Mathayo 14:1takriban 32 BK
Wakati huo, Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za Yesu,
- Mathayo 14:2takriban 32 BK
akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji; amefufuka kutoka kwa wafu! Hii ndiyo sababu nguvu za kutenda miujiza zinafanya kazi ndani yake.”
- Mathayo 14:3takriban 32 BK
Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga na kumweka gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake,
- Mathayo 14:4takriban 32 BK
kwa kuwa Yohana alikuwa amemwambia Herode: “Si halali kwako kuwa na huyo mwanamke.”
- Mathayo 14:5takriban 32 BK
Herode alitaka sana kumuua Yohana, lakini akaogopa watu, kwa maana walimtambua kuwa ni nabii.
- Mathayo 14:6takriban 32 BK
Katika siku ya kuadhimisha sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti wa Herodia alicheza mbele ya watu waliohudhuria, akamfurahisha sana Herode,
- Mathayo 14:7takriban 32 BK
kiasi kwamba aliahidi kwa kiapo kumpa huyo binti chochote angeomba.
- Mathayo 14:8takriban 32 BK
Huyo binti, akiwa amechochewa na mama yake, akasema, “Nipe kichwa cha Yohana Mbatizaji kwenye sinia.”
- Mathayo 14:9takriban 32 BK
Mfalme akasikitika, lakini kwa sababu ya viapo alivyoapa mbele ya wageni, akaamuru kwamba apatiwe ombi lake.
- Mathayo 14:10takriban 32 BK
Hivyo akaagiza Yohana Mbatizaji akatwe kichwa mle gerezani.
- Mathayo 14:11takriban 32 BK
Kichwa chake kikaletwa kwenye sinia, akapewa yule binti, naye akampelekea mama yake.
- Mathayo 14:12takriban 32 BK
Wanafunzi wa Yohana wakaja na kuuchukua mwili wake kwenda kuuzika. Kisha wakaenda wakamwambia Yesu.
- Mathayo 14:13takriban 32 BK
Yesu aliposikia yaliyokuwa yametukia, aliondoka kwa chombo akaenda mahali pasipo na watu ili awe peke yake. Lakini watu walipopata habari, wakamfuata kwa miguu kupitia nchi kavu kutoka miji.
- Mathayo 14:14takriban 32 BK
Yesu alipofika kando ya bahari, aliona makutano makubwa ya watu, akawahurumia na akawaponya wagonjwa wao.
- Mathayo 14:15takriban 32 BK
Ilipofika jioni, wanafunzi wake walienda kwake, wakamwambia, “Mahali hapa ni nyikani, na muda sasa umekwisha. Waage makutano ili waende zao vijijini wakajinunulie chakula.”
- Mathayo 14:16takriban 32 BK
Yesu akawaambia, “Hakuna sababu ya wao kuondoka. Ninyi wapeni chakula.”
- Mathayo 14:17takriban 32 BK
Wakamjibu, “Tuna mikate mitano na samaki wawili tu.”
- Mathayo 14:18takriban 32 BK
Akawaambia, “Nileteeni hivyo vitu hapa.”
- Mathayo 14:19takriban 32 BK
Yesu akaagiza makutano wakae chini kwenye nyasi. Akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akainua macho yake akatazama mbinguni, akavibariki na kuimega ile mikate. Kisha akawapa wanafunzi, nao wanafunzi wakawagawia makutano.
- Mathayo 14:20takriban 32 BK
Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
- Mathayo 14:21takriban 32 BK
Idadi ya watu waliokula walikuwa wanaume wapatao 5,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
- Mathayo 14:22takriban 32 BK
Mara Yesu akawaambia wanafunzi wake waingie kwenye mashua watangulie kwenda ngʼambo ya bahari, wakati yeye alikuwa akiwaaga wale makutano.