circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Mathayo 14:23takriban 32 BK
Baada ya kuwaaga, akaenda zake mlimani peke yake kuomba. Jioni ilipofika, Yesu alikuwa huko peke yake.
- Mathayo 14:24takriban 32 BK
Wakati huo ile mashua ilikuwa mbali kutoka nchi kavu ikisukwasukwa na mawimbi, kwa sababu upepo ulikuwa wa mbisho.
- Mathayo 14:25takriban 32 BK
Wakati wa zamu ya nne ya usiku, Yesu akawaendea wanafunzi wake akiwa anatembea juu ya maji.
- Mathayo 14:26takriban 32 BK
Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji, waliingiwa na hofu kuu, wakasema, “Ni mzimu.” Wakapiga yowe kwa kuogopa.
- Mathayo 14:27takriban 32 BK
Lakini mara Yesu akasema nao, akawaambia, “Jipeni moyo! Ni mimi. Msiogope.”
- Mathayo 14:28takriban 32 BK
Petro akamjibu, “Bwana, ikiwa ni wewe, niambie nije kwako nikitembea juu ya maji.”
- Mathayo 14:29takriban 32 BK
Yesu akamwambia, “Njoo.” Basi Petro akatoka kwenye chombo, akatembea juu ya maji kumwelekea Yesu.
- Mathayo 14:30takriban 32 BK
Lakini alipoona upepo mkali aliingiwa na hofu, naye akaanza kuzama, huku akipiga kelele, “Bwana, niokoe!”
- Mathayo 14:31takriban 32 BK
Mara Yesu akaunyoosha mkono wake na kumshika, akamwambia, “Wewe mwenye imani haba, kwa nini uliona shaka?”
- Mathayo 14:32takriban 32 BK
Nao walipoingia ndani ya mashua, upepo ukakoma.
- Mathayo 14:33takriban 32 BK
Ndipo wote waliokuwa ndani ya ile mashua wakamwabudu Yesu, wakisema, “Hakika, wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
- Mathayo 14:34takriban 32 BK
Walipokwisha kuvuka, wakafika nchi ya Genesareti.
- Mathayo 14:35takriban 32 BK
Watu wa eneo lile walipomtambua Yesu, walipeleka habari sehemu zote za jirani. Watu wakamletea wagonjwa wao wote,
- Mathayo 14:36takriban 32 BK
wakamsihi awaruhusu wagonjwa waguse tu pindo la vazi lake, nao wote waliomgusa, wakaponywa.
- Mathayo 15:1takriban 32 BK
Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamjia Yesu kutoka Yerusalemu na kumuuliza,
- Mathayo 15:2takriban 32 BK
“Mbona wanafunzi wako wanakiuka mapokeo ya wazee? Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla ya kula!”
- Mathayo 15:3takriban 32 BK
Yesu akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
- Mathayo 15:4takriban 32 BK
Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
- Mathayo 15:5takriban 32 BK
Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu,’
- Mathayo 15:6takriban 32 BK
basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu.
- Mathayo 15:7takriban 32 BK
Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:
- Mathayo 15:8takriban 32 BK
“ ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
- Mathayo 15:9takriban 32 BK
Huniabudu bure; nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’ ”
- Mathayo 15:10takriban 32 BK
Yesu akaita ule umati wa watu, akawaambia, “Sikilizeni na mwelewe:
- Mathayo 15:11takriban 32 BK
kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni kile kitokacho kinywani mwake.”