circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Mathayo 16:23takriban 32 BK
Lakini Yesu akageuka na kumwambia Petro, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
- Mathayo 16:24takriban 32 BK
Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
- Mathayo 16:25takriban 32 BK
Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayapata.
- Mathayo 16:26takriban 32 BK
Kwa maana, je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
- Mathayo 16:27takriban 32 BK
Kwa maana Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake, naye ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
- Mathayo 16:28takriban 32 BK
Nawaambia kweli, baadhi yenu hapa hawataonja mauti kabla ya kumwona Mwana wa Adamu akija katika Ufalme wake.”
- Mathayo 17:1takriban 32 BK
Siku sita baada ya jambo hili, Yesu akawachukua Petro, Yakobo na Yohana ndugu yake Yakobo, akawapeleka juu ya mlima mrefu peke yao.
- Mathayo 17:2takriban 32 BK
Wakiwa huko, Yesu alibadilika sura mbele yao. Uso wake ukangʼaa kama jua na nguo zake zikawa na weupe wa kuumiza macho.
- Mathayo 17:3takriban 32 BK
Ghafula wakawatokea mbele yao Mose na Eliya, wakizungumza na Yesu.
- Mathayo 17:4takriban 32 BK
Ndipo Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vyema sisi tukae hapa. Ukitaka, nitafanya vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.”
- Mathayo 17:5takriban 32 BK
Petro alipokuwa angali ananena, ghafula wingu lililongʼaa likawafunika, na sauti ikatoka kwenye hilo wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa naye sana. Msikieni yeye.”
- Mathayo 17:6takriban 32 BK
Wanafunzi waliposikia haya, wakaanguka chini kifudifudi, wakajawa na hofu.
- Mathayo 17:7takriban 32 BK
Lakini Yesu akaja na kuwagusa, akawaambia, “Inukeni na wala msiogope.”
- Mathayo 17:8takriban 32 BK
Walipoinua macho yao, hawakumwona mtu mwingine yeyote isipokuwa Yesu.
- Mathayo 17:9takriban 32 BK
Walipokuwa wakishuka kutoka mlimani, Yesu akawaagiza, “Msimwambie mtu yeyote mambo mliyoyaona hapa, mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuliwa kutoka kwa wafu.”
- Mathayo 17:10takriban 32 BK
Wale wanafunzi wakamuuliza, “Kwa nini basi walimu wa sheria husema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?”
- Mathayo 17:11takriban 32 BK
Yesu akawajibu, “Ni kweli, Eliya lazima aje kwanza, naye atatengeneza mambo yote.
- Mathayo 17:12takriban 32 BK
Lakini nawaambia, Eliya amekwisha kuja, nao hawakumtambua, bali walimtendea kila kitu walichotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu pia atateswa mikononi mwao.”
- Mathayo 17:13takriban 32 BK
Ndipo wale wanafunzi wakaelewa kuwa alikuwa anazungumza nao habari za Yohana Mbatizaji.
- Mathayo 17:14takriban 32 BK
Walipofika penye umati wa watu, mtu mmoja akamjia Yesu na kupiga magoti mbele yake, akasema,
- Mathayo 17:15takriban 32 BK
“Bwana, mhurumie mwanangu. Yeye ana kifafa na anateseka sana. Mara kwa mara huanguka kwenye moto au kwenye maji.
- Mathayo 17:16takriban 32 BK
Nilimleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumponya.”
- Mathayo 17:17takriban 32 BK
Yesu akajibu, “Enyi kizazi kisichoamini na kilichopotoka! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni mvulana hapa kwangu.”
- Mathayo 17:18takriban 32 BK
Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akamtoka yule kijana, naye akapona saa ile ile.
- Mathayo 17:19takriban 32 BK
Kisha wanafunzi wakamwendea Yesu wakiwa peke yao, wakamuuliza, “Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa?”