Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Mathayo 16:23takriban 32 BK

    Lakini Yesu akageuka na kumwambia Petro, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”

  2. Mathayo 16:24takriban 32 BK

    Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.

  3. Mathayo 16:25takriban 32 BK

    Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayapata.

  4. Mathayo 16:26takriban 32 BK

    Kwa maana, je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?

  5. Mathayo 16:27takriban 32 BK

    Kwa maana Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake, naye ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.

  6. Mathayo 16:28takriban 32 BK

    Nawaambia kweli, baadhi yenu hapa hawataonja mauti kabla ya kumwona Mwana wa Adamu akija katika Ufalme wake.”

  7. Mathayo 17:1takriban 32 BK

    Siku sita baada ya jambo hili, Yesu akawachukua Petro, Yakobo na Yohana ndugu yake Yakobo, akawapeleka juu ya mlima mrefu peke yao.

  8. Mathayo 17:2takriban 32 BK

    Wakiwa huko, Yesu alibadilika sura mbele yao. Uso wake ukangʼaa kama jua na nguo zake zikawa na weupe wa kuumiza macho.

  9. Mathayo 17:3takriban 32 BK

    Ghafula wakawatokea mbele yao Mose na Eliya, wakizungumza na Yesu.

  10. Mathayo 17:4takriban 32 BK

    Ndipo Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vyema sisi tukae hapa. Ukitaka, nitafanya vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.”

  11. Mathayo 17:5takriban 32 BK

    Petro alipokuwa angali ananena, ghafula wingu lililongʼaa likawafunika, na sauti ikatoka kwenye hilo wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa naye sana. Msikieni yeye.”

  12. Mathayo 17:6takriban 32 BK

    Wanafunzi waliposikia haya, wakaanguka chini kifudifudi, wakajawa na hofu.

  13. Mathayo 17:7takriban 32 BK

    Lakini Yesu akaja na kuwagusa, akawaambia, “Inukeni na wala msiogope.”

  14. Mathayo 17:8takriban 32 BK

    Walipoinua macho yao, hawakumwona mtu mwingine yeyote isipokuwa Yesu.

  15. Mathayo 17:9takriban 32 BK

    Walipokuwa wakishuka kutoka mlimani, Yesu akawaagiza, “Msimwambie mtu yeyote mambo mliyoyaona hapa, mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuliwa kutoka kwa wafu.”

  16. Mathayo 17:10takriban 32 BK

    Wale wanafunzi wakamuuliza, “Kwa nini basi walimu wa sheria husema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?”

  17. Mathayo 17:11takriban 32 BK

    Yesu akawajibu, “Ni kweli, Eliya lazima aje kwanza, naye atatengeneza mambo yote.

  18. Mathayo 17:12takriban 32 BK

    Lakini nawaambia, Eliya amekwisha kuja, nao hawakumtambua, bali walimtendea kila kitu walichotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu pia atateswa mikononi mwao.”

  19. Mathayo 17:13takriban 32 BK

    Ndipo wale wanafunzi wakaelewa kuwa alikuwa anazungumza nao habari za Yohana Mbatizaji.

  20. Mathayo 17:14takriban 32 BK

    Walipofika penye umati wa watu, mtu mmoja akamjia Yesu na kupiga magoti mbele yake, akasema,

  21. Mathayo 17:15takriban 32 BK

    “Bwana, mhurumie mwanangu. Yeye ana kifafa na anateseka sana. Mara kwa mara huanguka kwenye moto au kwenye maji.

  22. Mathayo 17:16takriban 32 BK

    Nilimleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumponya.”

  23. Mathayo 17:17takriban 32 BK

    Yesu akajibu, “Enyi kizazi kisichoamini na kilichopotoka! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni mvulana hapa kwangu.”

  24. Mathayo 17:18takriban 32 BK

    Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akamtoka yule kijana, naye akapona saa ile ile.

  25. Mathayo 17:19takriban 32 BK

    Kisha wanafunzi wakamwendea Yesu wakiwa peke yao, wakamuuliza, “Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa?”