circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Yohana 7:42takriban 33 BK
Je, Maandiko hayasemi kwamba Kristo atakuja kutoka jamaa ya Daudi na kutoka Bethlehemu, mji alioishi Daudi?”
- Yohana 7:43takriban 33 BK
Kwa hiyo watu wakagawanyika kwa ajili ya Yesu.
- Yohana 7:44takriban 33 BK
Baadhi yao walitaka kumkamata, lakini hakuna aliyethubutu kumgusa.
- Yohana 7:45takriban 33 BK
Hatimaye wale walinzi wa Hekalu wakarudi kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo waliokuwa wamewatuma ili kumkamata Yesu, wakaulizwa, “Mbona hamkumkamata?”
- Yohana 7:46takriban 33 BK
Wale walinzi wakajibu, “Kamwe hajanena mtu yeyote kama yeye anenavyo.”
- Yohana 7:47takriban 33 BK
Mafarisayo wakajibu, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
- Yohana 7:48takriban 33 BK
Je, kuna kiongozi yeyote au mmoja wa Mafarisayo ambaye amemwamini?
- Yohana 7:49takriban 33 BK
Lakini huu umati wa watu wasiojua Sheria ya Mose, wamelaaniwa.”
- Yohana 7:50takriban 33 BK
Ndipo Nikodemo, yule aliyekuwa amemwendea Yesu siku moja usiku, ambaye alikuwa mmoja wao akauliza,
- Yohana 7:51takriban 33 BK
“Je, sheria zetu zinaturuhusu kumhukumu mtu kabla ya kumsikiliza na kufahamu alilotenda?”
- Yohana 7:52takriban 33 BK
Wakamjibu, “Je, wewe pia unatoka Galilaya? Chunguza nawe utaona kwamba hakuna nabii atokae Galilaya!” [
- Yohana 7:53takriban 33 BK
Kisha wakaondoka, kila mtu akarudi nyumbani kwake.
- Yohana 8:1takriban 33 BK
Lakini Yesu akaenda katika Mlima wa Mizeituni.
- Yohana 8:2takriban 33 BK
Alfajiri na mapema Yesu akaja tena Hekaluni, watu wote wakakusanyika, akakaa akaanza kuwafundisha.
- Yohana 8:3takriban 33 BK
Walimu wa sheria na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote.
- Yohana 8:4takriban 33 BK
Wakamwambia Yesu, “Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini.
- Yohana 8:5takriban 33 BK
Katika sheria, Mose alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, mpaka wafe. Sasa wewe wasemaje?”
- Yohana 8:6takriban 33 BK
Walimuuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake.
- Yohana 8:7takriban 33 BK
Walipoendelea kumuulizauliza akainuka, akawaambia, “Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.”
- Yohana 8:8takriban 33 BK
Akainama tena na kuandika ardhini.
- Yohana 8:9takriban 33 BK
Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Yesu akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake.
- Yohana 8:10takriban 33 BK
Yesu akainuka na kumwambia, “Wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
- Yohana 8:11takriban 33 BK
Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako, kuanzia sasa usitende dhambi tena.”]
- Yohana 8:12takriban 33 BK
Kisha Yesu akasema nao tena akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
- Yohana 8:13takriban 33 BK
Mafarisayo wakamwambia, “Ushuhuda wako haukubaliki kwa kuwa unajishuhudia mwenyewe.”