Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Yohana 6:63takriban 32 BK

    Roho ndiye atiaye uzima, mwili haufai kitu. Maneno haya niliyowaambia ni Roho tena ni uzima.

  2. Yohana 6:64takriban 32 BK

    Lakini baadhi yenu hamwamini.” Kwa maana Yesu alifahamu tangu mwanzo wale ambao hawangemwamini miongoni mwao na yule ambaye angemsaliti.

  3. Yohana 6:65takriban 32 BK

    Akaendelea kusema, “Hii ndiyo sababu niliwaambia kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”

  4. Yohana 6:66takriban 32 BK

    Tangu wakati huo wafuasi wake wengi wakarejea nyuma wakaacha kumfuata.

  5. Yohana 6:67takriban 32 BK

    Hivyo Yesu akawauliza wale wanafunzi wake kumi na wawili, “Je, ninyi pia mnataka kuondoka?”

  6. Yohana 6:68takriban 32 BK

    Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tuondoke twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.

  7. Yohana 6:69takriban 32 BK

    Tunaamini na kujua kuwa wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu.”

  8. Yohana 6:70takriban 32 BK

    Ndipo Yesu akajibu, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Lakini mmoja wenu ni ibilisi.”

  9. Yohana 6:71takriban 32 BK

    (Hapa alikuwa anasema juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. Ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili, ndiye ambaye baadaye angemsaliti Yesu.)

  10. Yohana 7:1takriban 33 BK

    Baada ya mambo haya, Yesu alikwenda sehemu mbalimbali za Galilaya. Hakutaka kwenda Uyahudi kwa sababu Wayahudi huko walitaka kumuua.

  11. Yohana 7:2takriban 33 BK

    Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.

  12. Yohana 7:3takriban 33 BK

    Hivyo ndugu zake Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende Uyahudi ili wanafunzi Wako wapate kuona miujiza unayofanya.

  13. Yohana 7:4takriban 33 BK

    Mtu anayetaka kujulikana hafanyi mambo yake kwa siri. Kama unafanya mambo haya, jionyeshe kwa ulimwengu.”

  14. Yohana 7:5takriban 33 BK

    Hata ndugu zake mwenyewe hawakumwamini.

  15. Yohana 7:6takriban 33 BK

    Yesu akawaambia, “Wakati wangu bado haujawadia, lakini wakati wenu upo siku zote.

  16. Yohana 7:7takriban 33 BK

    Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini unanichukia mimi kwa sababu ninawashuhudia kwamba matendo yao ni maovu.

  17. Yohana 7:8takriban 33 BK

    Ninyi nendeni kwenye Sikukuu, lakini mimi sitahudhuria Sikukuu hii kwa sababu wakati wangu haujawadia.”

  18. Yohana 7:9takriban 33 BK

    Akiisha kusema hayo, akabaki Galilaya.

  19. Yohana 7:10takriban 33 BK

    Lakini ndugu zake walipokwisha kuondoka kwenda kwenye Sikukuu, yeye pia alikwenda lakini kwa siri.

  20. Yohana 7:11takriban 33 BK

    Wayahudi walikuwa wakimtafuta huko kwenye Sikukuu na kuulizana, “Yuko wapi huyu mtu?”

  21. Yohana 7:12takriban 33 BK

    Kulikuwa na minongʼono iliyoenea kumhusu Yesu katika umati wa watu, wakati wengine wakisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walikuwa wakisema, “La, yeye anawadanganya watu.”

  22. Yohana 7:13takriban 33 BK

    Lakini hakuna mtu yeyote aliyemsema waziwazi kumhusu kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi.

  23. Yohana 7:14takriban 33 BK

    Ilipokaribia katikati ya Sikukuu, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.

  24. Yohana 7:15takriban 33 BK

    Wayahudi wakastaajabia mafundisho yake wakasema, “Mtu huyu amepataje kujua mambo haya bila kufundishwa?”

  25. Yohana 7:16takriban 33 BK

    Ndipo Yesu akawajibu, “Mafundisho yangu si yangu mwenyewe, bali yanatoka kwake yeye aliyenituma.