circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Yohana 6:63takriban 32 BK
Roho ndiye atiaye uzima, mwili haufai kitu. Maneno haya niliyowaambia ni Roho tena ni uzima.
- Yohana 6:64takriban 32 BK
Lakini baadhi yenu hamwamini.” Kwa maana Yesu alifahamu tangu mwanzo wale ambao hawangemwamini miongoni mwao na yule ambaye angemsaliti.
- Yohana 6:65takriban 32 BK
Akaendelea kusema, “Hii ndiyo sababu niliwaambia kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”
- Yohana 6:66takriban 32 BK
Tangu wakati huo wafuasi wake wengi wakarejea nyuma wakaacha kumfuata.
- Yohana 6:67takriban 32 BK
Hivyo Yesu akawauliza wale wanafunzi wake kumi na wawili, “Je, ninyi pia mnataka kuondoka?”
- Yohana 6:68takriban 32 BK
Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tuondoke twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.
- Yohana 6:69takriban 32 BK
Tunaamini na kujua kuwa wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu.”
- Yohana 6:70takriban 32 BK
Ndipo Yesu akajibu, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Lakini mmoja wenu ni ibilisi.”
- Yohana 6:71takriban 32 BK
(Hapa alikuwa anasema juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. Ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili, ndiye ambaye baadaye angemsaliti Yesu.)
- Yohana 7:1takriban 33 BK
Baada ya mambo haya, Yesu alikwenda sehemu mbalimbali za Galilaya. Hakutaka kwenda Uyahudi kwa sababu Wayahudi huko walitaka kumuua.
- Yohana 7:2takriban 33 BK
Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
- Yohana 7:3takriban 33 BK
Hivyo ndugu zake Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende Uyahudi ili wanafunzi Wako wapate kuona miujiza unayofanya.
- Yohana 7:4takriban 33 BK
Mtu anayetaka kujulikana hafanyi mambo yake kwa siri. Kama unafanya mambo haya, jionyeshe kwa ulimwengu.”
- Yohana 7:5takriban 33 BK
Hata ndugu zake mwenyewe hawakumwamini.
- Yohana 7:6takriban 33 BK
Yesu akawaambia, “Wakati wangu bado haujawadia, lakini wakati wenu upo siku zote.
- Yohana 7:7takriban 33 BK
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini unanichukia mimi kwa sababu ninawashuhudia kwamba matendo yao ni maovu.
- Yohana 7:8takriban 33 BK
Ninyi nendeni kwenye Sikukuu, lakini mimi sitahudhuria Sikukuu hii kwa sababu wakati wangu haujawadia.”
- Yohana 7:9takriban 33 BK
Akiisha kusema hayo, akabaki Galilaya.
- Yohana 7:10takriban 33 BK
Lakini ndugu zake walipokwisha kuondoka kwenda kwenye Sikukuu, yeye pia alikwenda lakini kwa siri.
- Yohana 7:11takriban 33 BK
Wayahudi walikuwa wakimtafuta huko kwenye Sikukuu na kuulizana, “Yuko wapi huyu mtu?”
- Yohana 7:12takriban 33 BK
Kulikuwa na minongʼono iliyoenea kumhusu Yesu katika umati wa watu, wakati wengine wakisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walikuwa wakisema, “La, yeye anawadanganya watu.”
- Yohana 7:13takriban 33 BK
Lakini hakuna mtu yeyote aliyemsema waziwazi kumhusu kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi.
- Yohana 7:14takriban 33 BK
Ilipokaribia katikati ya Sikukuu, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
- Yohana 7:15takriban 33 BK
Wayahudi wakastaajabia mafundisho yake wakasema, “Mtu huyu amepataje kujua mambo haya bila kufundishwa?”
- Yohana 7:16takriban 33 BK
Ndipo Yesu akawajibu, “Mafundisho yangu si yangu mwenyewe, bali yanatoka kwake yeye aliyenituma.