Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Yohana 6:13takriban 32 BK

    Hivyo wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya ile mikate mitano ya shayiri na samaki wale wawili wadogo vilivyobakishwa na waliokula.

  2. Yohana 6:14takriban 32 BK

    Baada ya watu kuona muujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!”

  3. Yohana 6:15takriban 32 BK

    Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke yake.

  4. Yohana 6:16takriban 32 BK

    Ilipofika jioni, wanafunzi wake waliteremka kwenda baharini.

  5. Yohana 6:17takriban 32 BK

    Wakaingia kwenye mashua, wakaanza kuvuka bahari kwenda Kapernaumu. Wakati huu kulikuwa tayari giza na Yesu alikuwa hajajumuika nao.

  6. Yohana 6:18takriban 32 BK

    Bahari ikachafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.

  7. Yohana 6:19takriban 32 BK

    Wanafunzi walipokuwa wamekwenda mwendo wa karibu maili tatu au nne, walimwona Yesu akitembea juu ya maji akikaribia mashua, nao wakaogopa sana.

  8. Yohana 6:20takriban 32 BK

    Lakini Yesu akawaambia, “Ni mimi. Msiogope.”

  9. Yohana 6:21takriban 32 BK

    Ndipo wakamkaribisha kwa furaha ndani ya mashua, na mara wakafika ufuoni walikokuwa wakienda.

  10. Yohana 6:22takriban 32 BK

    Siku iliyofuata, wale watu waliokuwa wamebaki ngʼambo waliona kwamba palikuwepo na mashua moja tu na kwamba Yesu hakuwa ameondoka pamoja na wanafunzi wake, ila walikuwa wameondoka peke yao.

  11. Yohana 6:23takriban 32 BK

    Lakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia zikafika karibu na mahali pale walipokula mikate baada ya Bwana kumshukuru Mungu.

  12. Yohana 6:24takriban 32 BK

    Mara wale watu wakatambua kwamba Yesu hakuwepo hapo, wala wanafunzi wake. Wakaingia kwenye mashua hizo, wakaenda Kapernaumu ili kumtafuta Yesu.

  13. Yohana 6:25takriban 32 BK

    Walipomkuta Yesu ngʼambo ya bahari wakamuuliza, “Rabi, umefika lini huku?”

  14. Yohana 6:26takriban 32 BK

    Yesu akawajibu, “Amin, amin nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.

  15. Yohana 6:27takriban 32 BK

    Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.”

  16. Yohana 6:28takriban 32 BK

    Ndipo wakamuuliza, “Tufanye nini ili tupate kuitenda kazi ya Mungu?”

  17. Yohana 6:29takriban 32 BK

    Yesu akawajibu, “Kazi ya Mungu ndiyo hii: Mwaminini yeye aliyetumwa naye.”

  18. Yohana 6:30takriban 32 BK

    Hivyo wakamuuliza, “Utafanya ishara gani ya muujiza, ili tuione tukuamini? Utafanya jambo gani?

  19. Yohana 6:31takriban 32 BK

    Baba zetu walikula mana jangwani, kama ilivyoandikwa, ‘Aliwapa mikate kutoka mbinguni ili wale.’ ”

  20. Yohana 6:32takriban 32 BK

    Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, si Mose aliyewapa mikate kutoka mbinguni, bali Baba yangu ndiye anawapa mkate wa kweli kutoka mbinguni.

  21. Yohana 6:33takriban 32 BK

    Kwa maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.”

  22. Yohana 6:34takriban 32 BK

    Wakamwambia, “Bwana, kuanzia sasa tupatie huo mkate siku zote.”

  23. Yohana 6:35takriban 32 BK

    Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Yeye ajaye kwangu, hataona njaa kamwe na yeye aniaminiye, hataona kiu kamwe.

  24. Yohana 6:36takriban 32 BK

    Lakini kama nilivyowaambia, mmeniona lakini bado hamwamini.

  25. Yohana 6:37takriban 32 BK

    Wale wote anipao Baba watakuja kwangu na yeyote ajaye kwangu, sitamfukuzia nje kamwe.