circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Yohana 6:38takriban 32 BK
Kwa kuwa nimeshuka kutoka mbinguni si ili kufanya mapenzi yangu, bali mapenzi yake yeye aliyenituma.
- Yohana 6:39takriban 32 BK
Haya ndiyo mapenzi yake yeye aliyenituma, kwamba, nisimpoteze hata mmoja wa wale alionipa, bali niwafufue siku ya mwisho.
- Yohana 6:40takriban 32 BK
Kwa maana mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mmoja amtazamaye, Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele, nami nitawafufua siku ya mwisho.”
- Yohana 6:41takriban 32 BK
Wayahudi wakaanza kunungʼunika kwa kuwa alisema, “Mimi ndimi mkate ulioshuka kutoka mbinguni.”
- Yohana 6:42takriban 32 BK
Wakasema, “Huyu si Yesu, mwana wa Yosefu, ambaye baba yake na mama yake tunawajua? Anawezaje basi sasa kusema, ‘Nimeshuka kutoka mbinguni’?”
- Yohana 6:43takriban 32 BK
Hivyo Yesu akawaambia, “Acheni kunungʼunikiana ninyi kwa ninyi.
- Yohana 6:44takriban 32 BK
Hakuna mtu awezaye kuja kwangu kama asipovutwa na Baba aliyenituma, nami nitamfufua siku ya mwisho.
- Yohana 6:45takriban 32 BK
Imeandikwa katika Manabii, ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Yeyote amsikilizaye Baba na kujifunza kutoka kwake, huyo huja kwangu.
- Yohana 6:46takriban 32 BK
Hakuna mtu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yeye atokaye kwa Mungu, yeye ndiye peke yake aliyemwona Baba.
- Yohana 6:47takriban 32 BK
Amin, amin nawaambia, yeye anayeamini anao uzima wa milele.
- Yohana 6:48takriban 32 BK
Mimi ni mkate wa uzima.
- Yohana 6:49takriban 32 BK
Baba zenu walikula mana jangwani, lakini wakafa.
- Yohana 6:50takriban 32 BK
Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu yeyote akiula, hatakufa.
- Yohana 6:51takriban 32 BK
Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu yeyote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”
- Yohana 6:52takriban 32 BK
Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?”
- Yohana 6:53takriban 32 BK
Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.
- Yohana 6:54takriban 32 BK
Mtu yeyote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho.
- Yohana 6:55takriban 32 BK
Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
- Yohana 6:56takriban 32 BK
Yeyote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake.
- Yohana 6:57takriban 32 BK
Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.
- Yohana 6:58takriban 32 BK
Huu ndio mkate ushukao kutoka mbinguni, si kama ule mkate baba zenu waliokula nao wakafa. Lakini yeye aulaye mkate huu ataishi milele.”
- Yohana 6:59takriban 32 BK
Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika sinagogi huko Kapernaumu.
- Yohana 6:60takriban 32 BK
Wengi wa wafuasi wake waliposikia jambo hili wakasema, “Mafundisho haya ni magumu. Ni nani awezaye kuyapokea?”
- Yohana 6:61takriban 32 BK
Yesu alipojua kwamba wafuasi wake wananungʼunika kuhusu mafundisho yake, akawaambia, “Je, jambo hili limewaudhi?
- Yohana 6:62takriban 32 BK
Ingekuwaje basi kama mngemwona Mwana wa Adamu akipaa kwenda zake huko alipokuwa kwanza?