Rukia maudhui

circa AD 30–62

The Early Church

Pentecost ignites a movement; Peter, Paul, and countless others carry the gospel from Jerusalem to the ends of the earth.

1,007 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Matendo 10:15takriban 41 BK

    Ile sauti ikasema naye mara ya pili, “Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.”

  2. Matendo 10:16takriban 41 BK

    Jambo hili lilitokea mara tatu na ghafula ile nguo ikarudishwa mbinguni.

  3. Matendo 10:17takriban 41 BK

    Wakati Petro akiwa bado anajiuliza kuhusu maana ya maono haya, wale watu waliokuwa wametumwa na Kornelio wakaipata nyumba ya Simoni mtengenezaji wa ngozi wakawa wamesimama mbele ya lango.

  4. Matendo 10:18takriban 41 BK

    Wakabisha hodi na kuuliza kama Simoni aliyeitwa Petro alikuwa anaishi hapo.

  5. Matendo 10:19takriban 41 BK

    Wakati Petro akiwa anafikiria juu ya yale maono, Roho Mtakatifu akamwambia, “Simoni, wako watu watatu wanaokutafuta.

  6. Matendo 10:20takriban 41 BK

    Inuka na ushuke, usisite kwenda nao kwa kuwa mimi nimewatuma.”

  7. Matendo 10:21takriban 41 BK

    Petro akashuka na kuwaambia wale watu waliokuwa wametumwa kutoka kwa Kornelio, “Mimi ndiye mnayenitafuta. Mmekuja kwa sababu gani?”

  8. Matendo 10:22takriban 41 BK

    Wale watu wakamjibu, “Tumetumwa na Kornelio yule jemadari. Yeye ni mtu mwema anayemcha Mungu, na anaheshimiwa na Wayahudi wote. Yeye ameagizwa na malaika mtakatifu akukaribishe nyumbani kwake, ili asikilize maneno utakayomwambia.”

  9. Matendo 10:23takriban 41 BK

    Basi Petro akawakaribisha wakafuatana naye ndani, akawapa pa kulala. Kesho yake akaondoka pamoja nao, na baadhi ya ndugu kutoka Yafa wakafuatana naye.

  10. Matendo 10:24takriban 41 BK

    Siku iliyofuata wakawasili Kaisaria. Kornelio alikuwa akiwangoja pamoja na jamaa yake na marafiki zake wa karibu.

  11. Matendo 10:25takriban 41 BK

    Petro alipokuwa akiingia ndani, Kornelio alikuja kumlaki, akaanguka miguuni pake kwa heshima.

  12. Matendo 10:26takriban 41 BK

    Lakini Petro akamwinua akamwambia, “Simama, mimi ni mwanadamu tu.”

  13. Matendo 10:27takriban 41 BK

    Petro alipokuwa akizungumza naye akaingia ndani na kukuta watu wengi wamekusanyika.

  14. Matendo 10:28takriban 41 BK

    Akawaambia, “Mnajua kabisa kwamba ni kinyume cha sheria yetu Myahudi kuchangamana na mtu wa Mataifa au kumtembelea. Lakini Mungu amenionyesha kwamba nisimwite mtu yeyote kuwa najisi au asiye safi.

  15. Matendo 10:29takriban 41 BK

    Ndiyo sababu ulipotuma niitwe nilikuja bila kupinga lolote. Basi sasa naomba unieleze kwa nini umeniita?”

  16. Matendo 10:30takriban 41 BK

    Kornelio akajibu, “Siku nne zilizopita, nilikuwa nyumbani nikisali saa kama hii, saa tisa alasiri. Ghafula mtu aliyevaa nguo zilizongʼaa akasimama mbele yangu,

  17. Matendo 10:31takriban 41 BK

    akasema, ‘Kornelio, maombi yako yamesikiwa na sadaka zako kwa maskini zimekumbukwa mbele za Mungu.

  18. Matendo 10:32takriban 41 BK

    Basi tuma watu waende Yafa wakaulize mtu mmoja Simoni aitwaye Petro, yeye ni mgeni katika nyumba ya Simoni mtengenezaji ngozi, ambaye nyumba yake iko kando ya bahari.’

  19. Matendo 10:33takriban 41 BK

    Nilituma watu kwako mara moja, nawe umefanya vyema kuja. Basi sasa sisi sote tuko hapa mbele za Mungu kuyasikiliza yote ambayo Bwana amekuamuru kutuambia.”

  20. Matendo 10:34takriban 41 BK

    Ndipo Petro akafungua kinywa chake akasema, “Mungu hana upendeleo,

  21. Matendo 10:35takriban 41 BK

    Lakini katika kila taifa, kila mtu amchaye na kutenda yaliyo haki hukubaliwa naye.

  22. Matendo 10:36takriban 41 BK

    Ninyi mnajua ule ujumbe uliotumwa kwa Israeli, ukitangaza habari njema za amani kwa Yesu Kristo. Yeye ni Bwana wa wote.

  23. Matendo 10:37takriban 41 BK

    Mnajua yale yaliyotukia katika Uyahudi wote kuanzia Galilaya baada ya mahubiri ya Yohana Mbatizaji:

  24. Matendo 10:38takriban 41 BK

    Jinsi Mungu alivyomtia Yesu wa Nazareti mafuta katika Roho Mtakatifu na jinsi alivyokwenda huku na huko akitenda mema na kuponya wote waliokuwa wameonewa na nguvu za ibilisi, kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.

  25. Matendo 10:39takriban 41 BK

    “Sisi ni mashahidi wa mambo yote aliyoyafanya katika Uyahudi na Yerusalemu. Wakamuua kwa kumtundika msalabani.