Rukia maudhui

circa 1446 BC

Sinai & The Law

God meets Israel at Mount Sinai, reveals the Ten Commandments, and establishes the Tabernacle and the priestly covenant.

1,657 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Kutoka 30:16takriban 1491 KK

    Utapokea fedha ya upatanisho kutoka kwa Waisraeli na uzitumie kwa ajili ya huduma ya Hema la Kukutania. Itakuwa ni ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu.”

  2. Kutoka 30:17takriban 1491 KK

    Kisha Bwana akamwambia Mose,

  3. Kutoka 30:18takriban 1491 KK

    “Tengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kwa ajili ya kunawia. Liweke kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, kisha uweke maji ndani yake.

  4. Kutoka 30:19takriban 1491 KK

    Aroni na wanawe watanawa mikono na miguu yao kwa maji yatokayo katika hilo sinia.

  5. Kutoka 30:20takriban 1491 KK

    Wakati wowote wanapoingia katika Hema la Kukutania, watanawa kwa maji ili kwamba wasije wakafa. Pia, wanapokaribia madhabahu ili kuhudumu kwa kuleta sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto,

  6. Kutoka 30:21takriban 1491 KK

    watanawa mikono na miguu yao ili kwamba wasije wakafa. Hii itakuwa ni amri ya kudumu kwa ajili ya Aroni na wazao wake kwa vizazi vijavyo.”

  7. Kutoka 30:22takriban 1491 KK

    Kisha Bwana akamwambia Mose,

  8. Kutoka 30:23takriban 1491 KK

    “Chukua vikolezi bora vifuatavyo: shekeli 500 za manemane ya maji, shekeli 250 za mdalasini wenye harufu nzuri, shekeli 250 za miwa yenye harufu nzuri,

  9. Kutoka 30:24takriban 1491 KK

    shekeli 500 za aina nyingine ya mdalasini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, pia hini ya mafuta ya zeituni.

  10. Kutoka 30:25takriban 1491 KK

    Vitengeneze vikolezi hivi kuwa mafuta matakatifu ya upako yenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato. Yatakuwa mafuta matakatifu ya upako.

  11. Kutoka 30:26takriban 1491 KK

    Kisha yatumie kupaka hilo Hema la Kukutania, Sanduku la Ushuhuda,

  12. Kutoka 30:27takriban 1491 KK

    meza na vifaa vyake vyote, kinara cha taa na vifaa vyake vyote, madhabahu ya kufukizia uvumba,

  13. Kutoka 30:28takriban 1491 KK

    madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote na sinia pamoja na kitako chake.

  14. Kutoka 30:29takriban 1491 KK

    Utaviweka wakfu ili viwe vitakatifu sana na kila kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.

  15. Kutoka 30:30takriban 1491 KK

    “Mtie Aroni na wanawe mafuta na uwaweke wakfu ili waweze kunitumikia katika kazi ya ukuhani.

  16. Kutoka 30:31takriban 1491 KK

    Waambie Waisraeli, ‘Haya yatakuwa mafuta matakatifu yangu ya upako kwa vizazi vijavyo.

  17. Kutoka 30:32takriban 1491 KK

    Usiyamimine juu ya miili ya wanadamu wala usitengeneze mafuta ya aina nyingine kwa utaratibu huu. Ni mafuta matakatifu na ni lazima myaone kuwa ni matakatifu.

  18. Kutoka 30:33takriban 1491 KK

    Mtu yeyote atakayetengeneza manukato kama hayo na yeyote atakayeyamimina juu ya mtu yeyote ambaye si kuhani atakatiliwa mbali na watu wake.’ ”

  19. Kutoka 30:34takriban 1491 KK

    Kisha Bwana akamwambia Mose, “Chukua vikolezi vyenye harufu nzuri vifuatavyo: natafi, shekelethi, kelbena na uvumba safi vyote vikiwa na vipimo sawa,

  20. Kutoka 30:35takriban 1491 KK

    pia tengeneza mchanganyiko wa uvumba wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato. Utiwe chumvi ili upate kuwa safi na mtakatifu.

  21. Kutoka 30:36takriban 1491 KK

    Saga baadhi yake kuwa unga na uweke mbele ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Hema la Kukutania, mahali ambapo nitakutana nawe. Itakuwa takatifu sana kwenu.

  22. Kutoka 30:37takriban 1491 KK

    Msitengeneze uvumba mwingine wowote wa namna hii kwa ajili yenu wenyewe; uoneni kuwa ni mtakatifu kwa Bwana.

  23. Kutoka 30:38takriban 1491 KK

    Yeyote atakayetengeneza uvumba kama huu ili kufurahia harufu yake nzuri lazima akatiliwe mbali na watu wake.”

  24. Kutoka 31:1takriban 1491 KK

    Ndipo Bwana akamwambia Mose,

  25. Kutoka 31:2takriban 1491 KK

    “Tazama, nimemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,