God
Mistari inayomtaja God
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Nilishangilia pamoja na wale walioniambia, “Twende nyumbani ya Bwana.”
Huko ndiko makabila hukwea, makabila ya Bwana, kulisifu jina la Bwana kulingana na maagizo waliopewa Israeli.
Kwa ajili ya nyumba ya Bwana Mungu wetu, nitatafuta mafanikio yako.
Wimbo wa kwenda juu. Ninayainua macho yangu kwako, kwako wewe ambaye kiti chako cha enzi kiko mbinguni.
Kama vile macho ya watumwa yatazamavyo mkono wa bwana wao, kama vile macho ya mtumishi wa kike yatazamavyo mkono wa bibi yake, ndivyo macho yetu yamtazamavyo Bwana Mungu wetu, mpaka atakapotuhurumia.
Uturehemu, Ee Bwana, uturehemu, kwa maana tumevumilia dharau nyingi.
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
Wimbo wa kwenda juu. Wale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
Kama milima inavyozunguka Yerusalemu, ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake sasa na hata milele.
Ee Bwana, watendee mema walio wema, wale walio wanyofu wa moyo.
Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka, Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya. Amani iwe juu ya Israeli.
Wimbo wa kwenda juu. Bwana alipowarejeza mateka Sayuni, tulikuwa kama watu walioota ndoto.
Vinywa vyetu vilijaa kicheko, ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe. Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa, “Bwana amewatendea mambo makuu.”
Bwana ametutendea mambo makuu, nasi tumejaa furaha.
Ee Bwana, turejeshee watu wetu waliotekwa, kama vijito katika Negebu.
Wimbo wa kwenda juu. Wa Solomoni. Bwana asipoijenga nyumba, wajengao hufanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji, walinzi wakesha bure.
Mnajisumbua bure kuamka mapema na kuchelewa kulala, mkitaabikia chakula: kwa maana yeye huwapa usingizi wapenzi wake.
Wana ni urithi utokao kwa Bwana, watoto ni zawadi kutoka kwake.
Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.