God
Mistari inayomtaja God
Mwangazie mtumishi wako uso wako na unifundishe amri zako.
Chemchemi za machozi zinatiririka kutoka machoni yangu, kwa kuwa sheria yako haifuatwi.
Ee Bwana, wewe ni mwenye haki, sheria zako ni sahihi.
Sheria ulizoziweka ni za haki, ni za kuaminika kikamilifu.
Jitihada yangu imenidhoofisha, kwa kuwa adui zangu wanayapuuza maneno yako.
Ahadi zako zimejaribiwa kikamilifu, mtumishi wako anazipenda.
Ingawa ni mdogo na ninadharauliwa, sisahau mausia yako.
Haki yako ni ya milele, na sheria yako ni kweli.
Shida na dhiki zimenipata, lakini amri zako ni furaha yangu.
Sheria zako ni sahihi milele, hunipa ufahamu ili nipate kuishi.
Ee Bwana, ninakuita kwa moyo wangu wote, nami nitayatii maagizo yako.
Ninakuita; niokoe nami nitazishika sheria zako.
Ninaamka asubuhi na mapema na kukuomba msaada; nimeweka tumaini langu katika neno lako.
Sikufumba macho yangu usiku kucha, ili niweze kutafakari juu ya ahadi zako.
Usikie sauti yangu sawasawa na upendo wako, Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na sheria zako.
Wale wanaopanga mipango miovu wako karibu nami, lakini wako mbali na sheria yako.
Ee Bwana, hata hivyo wewe u karibu, na amri zako zote ni za kweli.
Tangu zamani nimejifunza kutoka shuhuda zako kwamba umezithibitisha ili zidumu milele.
Yaangalie mateso yangu, uniokoe, kwa kuwa sijasahau sheria yako.
Nitetee katika hali hii yangu na unikomboe, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na ahadi yako.
Wokovu uko mbali na waovu, kwa kuwa hawatafuti maagizo yako.
Ee Bwana, huruma zako ni kuu, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na sheria zako.
Adui wanaonitesa ni wengi, lakini mimi sitaziacha sheria zako.
Ninawatazama wasioamini kwa chuki, kwa kuwa hawalitii neno lako.
Tazama jinsi ninavyopenda mausia yako; Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na upendo wako.