God
Mistari inayomtaja God
Maneno yako yote ni kweli, sheria zako zote za haki ni za milele.
Watawala wamenitesa bila sababu, lakini moyo wangu unatetemeka kwa neno lako.
Nafurahia ahadi zako kama mtu aliyepata mateka mengi.
Ninachukia na kuchukizwa sana na uongo, lakini napenda sheria yako.
Ninakusifu mara saba kwa siku, kwa ajili ya sheria zako za haki.
Wanaopenda sheria yako wana amani tele, wala hakuna kitu kinachoweza kuwakwaza.
Ee Bwana, ninangojea wokovu wako, nami ninafuata amri zako,
Ninazitii sheria zako, kwa sababu ninazipenda mno.
Nimetii mausia yako na sheria zako, kwa kuwa njia zangu zote zinajulikana kwako.
Ee Bwana, kilio changu na kifike mbele zako, nipe ufahamu sawasawa na neno lako.
Maombi yangu na yafike mbele zako, niokoe sawasawa na ahadi yako.
Midomo yangu na ibubujike sifa, kwa kuwa unanifundisha maagizo yako.
Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, kwa kuwa amri zako zote ni za haki.
Mkono wako uwe tayari kunisaidia, kwa kuwa nimechagua mausia yako.
Ee Bwana, ninatamani wokovu wako, na sheria yako ni furaha yangu.
Nijalie kuishi ili nipate kukusifu, na sheria zako zinitegemeze.
Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea. Mtafute mtumishi wako, kwa kuwa sijasahau amri zako.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
Msaada wangu hutoka kwa Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
Hatauacha mguu wako uteleze, yeye akulindaye hatasinzia,
hakika, yeye alindaye Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi.
Bwana anakulinda, Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,
Bwana atakukinga na madhara yote, atayalinda maisha yako,
Bwana atakulinda unapoingia na unapotoka, tangu sasa na hata milele.