God
Mistari inayomtaja God
Bwana yuko pamoja nami, yeye ni msaidizi wangu. Nitawatazama adui zangu wakiwa wameshindwa.
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kumtumainia mwanadamu.
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kuwatumainia wakuu.
Mataifa yote yalinizunguka, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Walinizunguka pande zote, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Walinizunguka kama kundi la nyuki, lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo; kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka, lakini Bwana alinisaidia.
Bwana ni nguvu yangu na wimbo wangu, yeye amefanyika wokovu wangu.
Sauti za shangwe na ushindi zinavuma hemani mwa wenye haki: “Mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!
Mkono wa kuume wa Bwana umeinuliwa juu, mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!”
Sitakufa, bali nitaishi, nami nitatangaza yale Bwana aliyoyatenda.
Bwana ameniadhibu vikali, lakini hakuniacha nife.
Nifungulie malango ya haki, nami nitaingia na kumshukuru Bwana.
Hili ni lango la Bwana ambalo wenye haki wanaweza kuliingia.
Nitakushukuru, kwa kuwa ulinijibu, umekuwa wokovu wangu.
Bwana ametenda hili, nalo ni la kushangaza machoni petu.
Hii ndiyo siku Bwana aliyoifanya, tushangilie na kufurahi ndani yake.
Ee Bwana, tuokoe, Ee Bwana, utujalie mafanikio.
Heri yule ajaye kwa jina la Bwana. Kutoka nyumba ya Bwana tunakubariki.
Bwana ndiye Mungu, naye ametuangazia nuru yake. Mkiwa na matawi mkononi, unganeni kwenye maandamano ya sikukuu hadi kwenye pembe za madhabahu.
Wewe ni Mungu wangu, nitakushukuru, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza.
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Heri wale walio waadilifu katika njia zao, wanaoenenda katika sheria ya Bwana.
Heri wale wanaozishika shuhuda zake, wamtafutao kwa moyo wao wote.
Wasiofanya lolote lililo baya, wanaoenenda katika njia zake.