Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Shem: Descendants of

70 mistari · 4 vipengele

Mistari kuhusu Descendants of

Chuja kwa kitabu
  1. Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.

  2. Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.

  3. Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.

  4. Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.

  5. Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.

  6. Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.

  7. Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,

  8. Hadoramu, Uzali, Dikla,

  9. Obali, Abimaeli, Sheba,

  10. Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.

  11. Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.

  12. Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.

  13. Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.

  14. Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

  15. Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.

  16. Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

  17. Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.

  18. Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

  19. Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.

  20. Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

  21. Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.

  22. Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

  23. Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.

  24. Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

  25. Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.