Mistari ya Biblia kuhusu Journey of Israel Through The Desert: The people terrified and rebel
Mistari kuhusu The people terrified and rebel
Usiku ule watu wote wa jumuiya walipaza sauti zao na kulia kwa sauti kuu.
Waisraeli wote wakanungʼunika dhidi ya Mose na Aroni, nalo kusanyiko lote wakawaambia, “Laiti tungekuwa tumefia humo nchi ya Misri! Au humu kwenye hili jangwa!
Kwa nini Bwana anatuleta katika nchi hii ili tufe kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watachukuliwa kama nyara. Je, isingekuwa bora kwetu kurudi Misri?”
Wakasemezana wao kwa wao, “Inatupasa kumchagua kiongozi na kurudi Misri.”