Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Birds: Habits of

11 mistari · 107 vipengele

Mistari kuhusu Habits of

  1. “Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.

  2. Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,

  3. bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.

  4. Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,

  5. kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.

  6. Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.

  7. “Je, mwewe huruka kwa hekima yako na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?

  8. Je, tai hupaa juu kwa amri yako na kujenga kiota chake mahali pa juu?

  9. Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku; majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.

  10. Kutoka huko hutafuta chakula chake; macho yake hukiona kutoka mbali.

  11. Makinda yake hujilisha damu, na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”