Mistari ya Biblia kuhusu Birds: What species were unclean
Mistari kuhusu What species were unclean
“ ‘Wafuatao ndio ndege watakaokuwa machukizo kwenu, hivyo msiwale kwa sababu ni chukizo: tai, furukombe, kipungu,
mwewe mwekundu, aina zote za mwewe mweusi,
aina zote za kunguru,
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga, shakwe, aina zote za kipanga,
bundi, mnandi, bundi mkubwa,
mumbi, mwari, nderi,
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
“ ‘Wadudu wote warukao ambao hutembea kwa miguu minne watakuwa chukizo kwenu.
Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
kunguru wa aina yoyote,
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
bundi, mumbi, bundi mkubwa,
mwari, nderi, mnandi,
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.