Rukia maudhui

circa 1010–970 BC

The Reign of David

David unites the tribes, conquers Jerusalem, and establishes Israel's golden age—even through deep personal failure.

1,230 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 2 Samweli 21:18takriban 1018 KK

    Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.

  2. 2 Samweli 21:19takriban 1018 KK

    Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.

  3. 2 Samweli 21:20takriban 1018 KK

    Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.

  4. 2 Samweli 21:21takriban 1018 KK

    Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.

  5. 2 Samweli 21:22takriban 1018 KK

    Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.

  6. 2 Samweli 22:1takriban 1018 KK

    Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.

  7. 2 Samweli 22:2takriban 1018 KK

    Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,

  8. 2 Samweli 22:3takriban 1018 KK

    Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.

  9. 2 Samweli 22:4takriban 1018 KK

    Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.

  10. 2 Samweli 22:5takriban 1018 KK

    “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.

  11. 2 Samweli 22:6takriban 1018 KK

    Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili.

  12. 2 Samweli 22:7takriban 1018 KK

    Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.

  13. 2 Samweli 22:8takriban 1018 KK

    “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.

  14. 2 Samweli 22:9takriban 1018 KK

    Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.

  15. 2 Samweli 22:10takriban 1018 KK

    Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.

  16. 2 Samweli 22:11takriban 1018 KK

    Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.

  17. 2 Samweli 22:12takriban 1018 KK

    Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.

  18. 2 Samweli 22:13takriban 1018 KK

    Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.

  19. 2 Samweli 22:14takriban 1018 KK

    Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.

  20. 2 Samweli 22:15takriban 1018 KK

    Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.

  21. 2 Samweli 22:16takriban 1018 KK

    Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.

  22. 2 Samweli 22:17takriban 1018 KK

    “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.

  23. 2 Samweli 22:18takriban 1018 KK

    Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.

  24. 2 Samweli 22:19takriban 1018 KK

    Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.

  25. 2 Samweli 22:20takriban 1018 KK

    Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.