circa 1010–970 BC
The Reign of David
David unites the tribes, conquers Jerusalem, and establishes Israel's golden age—even through deep personal failure.
Mistari ya kipindi hiki
- 2 Samweli 22:21takriban 1018 KK
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
- 2 Samweli 22:22takriban 1018 KK
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
- 2 Samweli 22:23takriban 1018 KK
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
- 2 Samweli 22:24takriban 1018 KK
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
- 2 Samweli 22:25takriban 1018 KK
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
- 2 Samweli 22:26takriban 1018 KK
“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
- 2 Samweli 22:27takriban 1018 KK
kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
- 2 Samweli 22:28takriban 1018 KK
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
- 2 Samweli 22:29takriban 1018 KK
Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
- 2 Samweli 22:30takriban 1018 KK
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
- 2 Samweli 22:31takriban 1018 KK
“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
- 2 Samweli 22:32takriban 1018 KK
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
- 2 Samweli 22:33takriban 1018 KK
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
- 2 Samweli 22:34takriban 1018 KK
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
- 2 Samweli 22:35takriban 1018 KK
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
- 2 Samweli 22:36takriban 1018 KK
Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
- 2 Samweli 22:37takriban 1018 KK
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
- 2 Samweli 22:38takriban 1018 KK
“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
- 2 Samweli 22:39takriban 1018 KK
Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
- 2 Samweli 22:40takriban 1018 KK
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
- 2 Samweli 22:41takriban 1018 KK
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
- 2 Samweli 22:42takriban 1018 KK
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
- 2 Samweli 22:43takriban 1018 KK
Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
- 2 Samweli 22:44takriban 1018 KK
“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
- 2 Samweli 22:45takriban 1018 KK
nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.