circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Luka 1:27takriban 5 KK
kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
- Luka 1:28takriban 5 KK
Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
- Luka 1:29takriban 5 KK
Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
- Luka 1:30takriban 5 KK
Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
- Luka 1:31takriban 5 KK
Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
- Luka 1:32takriban 5 KK
Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
- Luka 1:33takriban 5 KK
Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”
- Luka 1:34takriban 5 KK
Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
- Luka 1:35takriban 5 KK
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
- Luka 1:36takriban 5 KK
Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
- Luka 1:37takriban 5 KK
Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
- Luka 1:38takriban 5 KK
Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
- Luka 1:39takriban 5 KK
Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
- Luka 1:40takriban 5 KK
Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
- Luka 1:41takriban 5 KK
Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
- Luka 1:42takriban 5 KK
akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
- Luka 1:43takriban 5 KK
Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
- Luka 1:44takriban 5 KK
Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
- Luka 1:45takriban 5 KK
Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
- Luka 1:46takriban 5 KK
Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
- Luka 1:47takriban 5 KK
nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
- Luka 1:48takriban 5 KK
kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
- Luka 1:49takriban 5 KK
kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
- Luka 1:50takriban 5 KK
Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
- Luka 1:51takriban 5 KK
Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.