Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 1:27takriban 5 KK

    kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.

  2. Luka 1:28takriban 5 KK

    Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”

  3. Luka 1:29takriban 5 KK

    Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”

  4. Luka 1:30takriban 5 KK

    Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.

  5. Luka 1:31takriban 5 KK

    Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.

  6. Luka 1:32takriban 5 KK

    Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.

  7. Luka 1:33takriban 5 KK

    Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”

  8. Luka 1:34takriban 5 KK

    Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”

  9. Luka 1:35takriban 5 KK

    Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.

  10. Luka 1:36takriban 5 KK

    Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.

  11. Luka 1:37takriban 5 KK

    Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”

  12. Luka 1:38takriban 5 KK

    Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.

  13. Luka 1:39takriban 5 KK

    Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.

  14. Luka 1:40takriban 5 KK

    Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.

  15. Luka 1:41takriban 5 KK

    Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,

  16. Luka 1:42takriban 5 KK

    akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.

  17. Luka 1:43takriban 5 KK

    Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?

  18. Luka 1:44takriban 5 KK

    Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.

  19. Luka 1:45takriban 5 KK

    Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”

  20. Luka 1:46takriban 5 KK

    Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,

  21. Luka 1:47takriban 5 KK

    nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,

  22. Luka 1:48takriban 5 KK

    kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,

  23. Luka 1:49takriban 5 KK

    kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.

  24. Luka 1:50takriban 5 KK

    Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.

  25. Luka 1:51takriban 5 KK

    Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.