circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Luka 1:52takriban 5 KK
Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
- Luka 1:53takriban 5 KK
Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
- Luka 1:54takriban 5 KK
Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
- Luka 1:55takriban 5 KK
Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.”
- Luka 1:56takriban 5 KK
Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
- Luka 1:57takriban 5 KK
Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
- Luka 1:58takriban 5 KK
Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
- Luka 1:59takriban 5 KK
Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
- Luka 1:60takriban 5 KK
Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
- Luka 1:61takriban 5 KK
Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
- Luka 1:62takriban 5 KK
Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
- Luka 1:63takriban 5 KK
Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
- Luka 1:64takriban 5 KK
Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
- Luka 1:65takriban 5 KK
Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
- Luka 1:66takriban 5 KK
Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
- Luka 1:67takriban 5 KK
Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
- Luka 1:68takriban 5 KK
“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
- Luka 1:69takriban 5 KK
Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
- Luka 1:70takriban 5 KK
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani,
- Luka 1:71takriban 5 KK
kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
- Luka 1:72takriban 5 KK
ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
- Luka 1:73takriban 5 KK
kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
- Luka 1:74takriban 5 KK
kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
- Luka 1:75takriban 5 KK
katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
- Luka 1:76takriban 5 KK
“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,