Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 1:52takriban 5 KK

    Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.

  2. Luka 1:53takriban 5 KK

    Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.

  3. Luka 1:54takriban 5 KK

    Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu

  4. Luka 1:55takriban 5 KK

    Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.”

  5. Luka 1:56takriban 5 KK

    Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.

  6. Luka 1:57takriban 5 KK

    Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.

  7. Luka 1:58takriban 5 KK

    Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.

  8. Luka 1:59takriban 5 KK

    Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.

  9. Luka 1:60takriban 5 KK

    Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”

  10. Luka 1:61takriban 5 KK

    Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”

  11. Luka 1:62takriban 5 KK

    Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.

  12. Luka 1:63takriban 5 KK

    Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”

  13. Luka 1:64takriban 5 KK

    Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.

  14. Luka 1:65takriban 5 KK

    Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.

  15. Luka 1:66takriban 5 KK

    Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.

  16. Luka 1:67takriban 5 KK

    Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:

  17. Luka 1:68takriban 5 KK

    “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.

  18. Luka 1:69takriban 5 KK

    Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,

  19. Luka 1:70takriban 5 KK

    kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani,

  20. Luka 1:71takriban 5 KK

    kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:

  21. Luka 1:72takriban 5 KK

    ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,

  22. Luka 1:73takriban 5 KK

    kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:

  23. Luka 1:74takriban 5 KK

    kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu

  24. Luka 1:75takriban 5 KK

    katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.

  25. Luka 1:76takriban 5 KK

    “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,