Rukia maudhui

circa AD 30–62

The Early Church

Pentecost ignites a movement; Peter, Paul, and countless others carry the gospel from Jerusalem to the ends of the earth.

1,007 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Matendo 13:37takriban 45 BK

    Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu hakuona uharibifu.

  2. Matendo 13:38takriban 45 BK

    “Kwa hiyo ndugu zangu, nataka ninyi mjue kwamba kwa kupitia huyu Yesu msamaha wa dhambi unatangazwa kwenu.

  3. Matendo 13:39takriban 45 BK

    Kwa kupitia yeye, kila mtu amwaminiye anahesabiwa haki kwa kila kitu ambacho asingeweza kuhesabiwa haki kwa sheria ya Mose.

  4. Matendo 13:40takriban 45 BK

    Kwa hiyo jihadharini ili yale waliyosema manabii yasiwapate:

  5. Matendo 13:41takriban 45 BK

    “ ‘Angalieni, enyi wenye dhihaka, mkastaajabu, mkaangamie, kwa maana nitatenda jambo wakati wenu ambalo hamtasadiki, hata kama mtu akiwaambia.’ ”

  6. Matendo 13:42takriban 45 BK

    Paulo na Barnaba walipokuwa wakitoka nje ya sinagogi, watu wakawaomba wazungumze tena mambo hayo Sabato iliyofuata.

  7. Matendo 13:43takriban 45 BK

    Baada ya kusanyiko la Sinagogi kutawanyika, wengi wa Wayahudi na waongofu wa dini ya Kiyahudi wakawafuata Paulo na Barnaba, wakazungumza nao na kuwahimiza wadumu katika neema ya Mungu.

  8. Matendo 13:44takriban 45 BK

    Sabato iliyofuata, karibu watu wote wa mji walikuja kusikiliza neno la Bwana.

  9. Matendo 13:45takriban 45 BK

    Lakini Wayahudi walipoona ule umati mkubwa wa watu walijawa na wivu, wakayakanusha maneno Paulo aliyokuwa akisema.

  10. Matendo 13:46takriban 45 BK

    Ndipo Paulo na Barnaba wakawajibu kwa ujasiri, wakisema, “Ilitupasa kunena nanyi neno la Mungu kwanza. Lakini kwa kuwa mmelikataa, mkajihukumu wenyewe kuwa hamstahili uzima wa milele, sasa tunawageukia watu wa Mataifa.

  11. Matendo 13:47takriban 45 BK

    Kwa maana hili ndilo Bwana alilotuamuru: “ ‘Nimewafanya ninyi kuwa nuru kwa watu wa Mataifa, ili mpate kuuleta wokovu hadi miisho ya dunia.’ ”

  12. Matendo 13:48takriban 45 BK

    Watu wa Mataifa waliposikia haya wakafurahi na kulitukuza neno la Bwana; nao wote waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini.

  13. Matendo 13:49takriban 45 BK

    Neno la Bwana likaenea katika eneo lile lote.

  14. Matendo 13:50takriban 45 BK

    Lakini Wayahudi wakawachochea wanawake wenye kumcha Mungu, wenye vyeo pamoja na watu maarufu katika mji, wakachochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na kuwafukuza kutoka eneo hilo.

  15. Matendo 13:51takriban 45 BK

    Hivyo Paulo na Barnaba wakakungʼuta mavumbi ya miguu yao ili kuwapinga, nao wakaenda Ikonio.

  16. Matendo 13:52takriban 45 BK

    Wanafunzi wakajawa na furaha na Roho Mtakatifu.

  17. Matendo 14:1takriban 46 BK

    Huko Ikonio Paulo na Barnaba waliingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi kama ilivyokuwa desturi yao. Huko wakahubiri kwa uwezo mkubwa kiasi kwamba Wayahudi pamoja na watu wa Mataifa wakaamini.

  18. Matendo 14:2takriban 46 BK

    Lakini wale Wayahudi waliokataa kuamini, wakawachochea watu wa Mataifa, wakatia chuki ndani ya mioyo yao dhidi ya wale walioamini.

  19. Matendo 14:3takriban 46 BK

    Hivyo Paulo na Barnaba wakakaa huko kwa muda wa kutosha wakihubiri kwa ujasiri juu ya Bwana, ambaye alithibitisha ujumbe wa neema yake kwa kuwawezesha kufanya ishara na miujiza.

  20. Matendo 14:4takriban 46 BK

    Lakini watu wa mji ule waligawanyika, wengine wakakubaliana na Wayahudi na wengine na mitume.

  21. Matendo 14:5takriban 46 BK

    Watu wa Mataifa na Wayahudi wakajiunga na baadhi ya viongozi, wakafanya mpango wa kuwatendea mitume mabaya na kuwapiga mawe.

  22. Matendo 14:6takriban 46 BK

    Lakini mitume walipopata habari hizi wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia na sehemu zilizopakana nayo.

  23. Matendo 14:7takriban 46 BK

    Huko wakaendelea kuhubiri habari njema.

  24. Matendo 14:8takriban 46 BK

    Katika mji wa Listra, alikuwako kiwete, ambaye alikuwa amelemaa tangu kuzaliwa na hakuwa ametembea kamwe.

  25. Matendo 14:9takriban 46 BK

    Alimsikiliza Paulo alipokuwa akihubiri. Paulo alipomtazama akaona ana imani ya kuponywa.