God
Mistari inayomtaja God
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
Zaburi ya Asafu. Mungu anaongoza kusanyiko kuu, anatoa hukumu miongoni mwa “miungu”:
“Nilisema, ‘Ninyi ni “miungu”; ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Sana.’
Ee Mungu, inuka uihukumu nchi, kwa kuwa mataifa yote ni urithi wako.
Wimbo. Zaburi ya Asafu. Ee Mungu, usinyamaze kimya, usinyamaze, Ee Mungu, usitulie.
Tazama watesi wako wanafanya fujo, jinsi adui zako wanavyoinua vichwa vyao.
Kwa hila, wanafanya shauri dhidi ya watu wako, wanafanya shauri baya dhidi ya wale unaowapenda.
Kwa nia moja wanapanga mashauri mabaya pamoja, wanafanya muungano dhidi yako,
ambao walisema, “Na tumiliki nchi ya malisho ya Mungu.”
Ee Mungu wangu, wapeperushe kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi yapeperushwayo na upepo.
wafuatilie kwa tufani yako na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.