- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi44
Listen to this chapter
0:00
0:00
Kukumbuka Wokovu wa Mungu wa Zamani
1
Kwa mwimbishaji. Utenzi wa wana wa Kora. Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametueleza yale uliyotenda katika siku zao, siku za kale.
2
Kwa mkono wako uliwafukuza mataifa na ukawapanda baba zetu, uliangamiza mataifa na kuwastawisha baba zetu.
3
Sio kwa upanga wao waliipata nchi, wala si mkono wao uliwapatia ushindi; ilikuwa ni kitanga cha mkono wako wa kuume, na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwapenda.
4
Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu, unayeamuru ushindi kwa Yakobo.
5
Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu; kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu.
6
Siutumaini upinde wangu, upanga wangu hauniletei ushindi;
7
bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu, unawaaibisha watesi wetu.
8
Katika Mungu wetu tunajivuna mchana kutwa, nasi tutalisifu jina lako milele.
Hali ya Sasa ya Kushindwa na Kukataliwa
9
Lakini sasa umetukataa na kutudhili, wala huendi tena na jeshi letu.
10
Umetufanya turudi nyuma mbele ya adui, nao watesi wetu wametuteka nyara.
11
Umetuacha tutafunwe kama kondoo na umetutawanya katika mataifa.
12
Umewauza watu wako kwa fedha kidogo, wala hukupata faida yoyote kwa mauzo yao.
13
Umetufanya lawama kwa jirani zetu, dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka.
14
Umetufanya kuwa mithali miongoni mwa mataifa, mataifa hutikisa vichwa vyao.
15
Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa, na uso wangu umejaa aibu tele,
16
kwa ajili ya dhihaka ya wale wanaonilaumu na kunitukana, kwa sababu ya adui, ambaye anatamani kulipiza kisasi.
Tamko la Uaminifu kwa Agano
17
Hayo yote yametutokea, ingawa tulikuwa hatujakusahau wala hatujaenda kinyume na agano lako.
18
Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma; nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako.
19
Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha, na ukatufunika kwa giza nene.
20
Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni,
21
je, Mungu hangaligundua hili, kwa kuwa anazijua siri za moyo?
22
Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.
Ombi la Kukata Tamaa kwa Mungu Kuingilia
23
Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? Zinduka! Usitukatae milele.
24
Kwa nini unauficha uso wako na kusahau taabu na mateso yetu?
25
Tumeshushwa hadi mavumbini, miili yetu imegandamana na ardhi.
26
Inuka na utusaidie, utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note