Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Select Readings

802 mistari · 47 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Watu wasiomjua Mungu ndio wanaoshindania hayo, lakini Baba yenu wa mbinguni anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.

  2. Lakini utafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake, na haya yote atawapa pia.

  3. Kwa hiyo msiwe na wasiwasi kuhusu kesho, kwa sababu kesho itajitaabikia yenyewe. Yatosha kwa siku masumbufu yake.

  4. “Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni, bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

  5. Wengi wataniambia siku ile, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo wachafu na kufanya miujiza mingi?’

  6. Ndipo nitakapowaambia wazi, ‘Sikuwajua kamwe. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’

  7. “Kwa hiyo kila mtu ayasikiaye haya maneno yangu na kuyatenda, ni kama mtu mwenye busara aliyejenga nyumba yake kwenye mwamba.

  8. Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba. Lakini haikuanguka; kwa sababu msingi wake ulikuwa kwenye mwamba.

  9. Naye kila anayesikia haya maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu mjinga aliyejenga nyumba yake kwenye mchanga.

  10. Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, nao upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba, nayo ikaanguka kwa kishindo kikubwa.”

  11. Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,

  12. nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,

  13. kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,

  14. kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.

  15. Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.

  16. Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.

  17. Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.

  18. Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.

  19. Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu

  20. Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.”

  21. Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.

  22. Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:

  23. “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.

  24. Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,

  25. kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani,