Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Beasts

26 mistari · 90 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. “ ‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.

  2. Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.

  3. Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.

  4. Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.

  5. Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.

  6. Punda alipomwona malaika wa Bwana, alilala chini Balaamu angali amempanda, naye Balaamu akakasirika na kumpiga kwa fimbo yake.

  7. Kisha Bwana akakifungua kinywa cha punda, akamwambia Balaamu, “Nimekutendea nini kinachokufanya unipige mara hizi tatu?”

  8. Balaamu akamjibu punda, “Umenifanya mjinga! Kama ningelikuwa na upanga mkononi mwangu, ningelikuua sasa hivi.”

  9. Punda akamwambia Balaamu, “Je, mimi si punda wako mwenyewe, ambaye umenipanda siku zote, hadi leo? Je, nimekuwa na tabia ya kufanya hivi kwako?” Akajibu, “Hapana.”

  10. Kisha Bwana akafungua macho ya Balaamu, naye akamwona malaika wa Bwana amesimama barabarani akiwa ameufuta upanga wake. Balaamu akainama, akaanguka kifudifudi.

  11. Malaika wa Bwana akamuuliza Balaamu, “Kwa nini umempiga punda wako mara tatu hizi? Nimekuja kukuzuia kwa sababu njia yako imepotoka mbele yangu.

  12. “Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru? Ni nani aliyezifungua kamba zake?

  13. Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake, nchi ya chumvi kuwa makao yake.

  14. Huzicheka ghasia za mji, wala hasikii kelele za mwendesha gari.

  15. Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho na kutafuta kila kitu kibichi.

  16. “Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?

  17. Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?

  18. Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.

  19. Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.

  20. Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.

  21. Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.

  22. Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.

  23. Lakini mwanadamu, licha ya utajiri wake, hadumu; anafanana na mnyama aangamiaye.

  24. Hii ndiyo hatima ya wale wanaojitumainia wenyewe, pia ya wafuasi wao, waliothibitisha misemo yao.

  25. Kama kondoo, wamewekewa kwenda kaburini, nacho kifo kitawala. Wanyofu watawatawala asubuhi, maumbile yao yataozea kaburini, mbali na majumba yao makubwa ya fahari.