Mistari ya Biblia kuhusu Beasts: Not eaten
Mistari kuhusu Not eaten
“ ‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.
Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.
Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.