Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 9:44takriban 32 BK

    “Sikilizeni kwa makini haya nitakayowaambia sasa: Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu.”

  2. Luka 9:45takriban 32 BK

    Lakini wao hawakuelewa alimaanisha nini. Maana ya maneno hayo ilifichika kwao, hivyo hawakuyaelewa, nao wakaogopa kumuuliza maana yake.

  3. Luka 9:46takriban 32 BK

    Kukazuka mabishano miongoni mwa wanafunzi kuhusu ni nani miongoni mwao atakayekuwa mkuu kuliko wote.

  4. Luka 9:47takriban 32 BK

    Lakini Yesu akayatambua mawazo yao, naye akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kando yake.

  5. Luka 9:48takriban 32 BK

    Kisha akawaambia, “Yeyote amkaribishaye mtoto huyu mdogo kwa Jina langu, anikaribisha mimi, na yeyote atakayenikaribisha mimi, atakuwa amemkaribisha yeye aliyenituma. Kwa maana yeye aliye mdogo miongoni mwenu, ndiye aliye mkuu kuliko wote.”

  6. Luka 9:49takriban 32 BK

    Yohana akasema, “Bwana, tumemwona mtu akitoa pepo wachafu kwa jina lako, nasi tukamzuia, kwa sababu yeye si mmoja wetu.”

  7. Luka 9:50takriban 32 BK

    Yesu akasema, “Msimzuie, kwa sababu yeyote ambaye si kinyume nanyi, yu upande wenu.”

  8. Luka 9:51takriban 32 BK

    Wakati ulipokaribia wa yeye kuchukuliwa mbinguni, alikaza uso wake kwenda Yerusalemu.

  9. Luka 9:52takriban 32 BK

    Akatuma watu wamtangulie, nao wakaenda katika kijiji kimoja cha Samaria kumwandalia kila kitu;

  10. Luka 9:53takriban 32 BK

    lakini watu wa kijiji kile hawakumkaribisha kwa sababu alikuwa anakwenda zake Yerusalemu.

  11. Luka 9:54takriban 32 BK

    Wanafunzi wake, yaani Yakobo na Yohana, walipoona hayo, wakasema: “Bwana, unataka tuagize moto kutoka mbinguni ili uwaangamize?”

  12. Luka 9:55takriban 32 BK

    Yesu akageuka na kuwakemea,

  13. Luka 9:56takriban 32 BK

    nao wakaenda kijiji kingine.

  14. Luka 9:57takriban 32 BK

    Walipokuwa njiani wakienda, mtu mmoja akamwambia Yesu, “Nitakufuata kokote uendako.”

  15. Luka 9:58takriban 32 BK

    Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”

  16. Luka 9:59takriban 32 BK

    Yesu akamwambia mtu mwingine, “Nifuate.” Mtu huyo akamjibu, “Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu.”

  17. Luka 9:60takriban 32 BK

    Yesu akamwambia, “Waache wafu wawazike wafu wao, bali wewe nenda ukautangaze Ufalme wa Mungu.”

  18. Luka 9:61takriban 32 BK

    Mtu mwingine akamwambia, “Bwana, nitakufuata lakini naomba kwanza nikawaage jamaa yangu.”

  19. Luka 9:62takriban 32 BK

    Yesu akamwambia, “Mtu yeyote atiaye mkono wake kulima, kisha akatazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.”

  20. Luka 10:1takriban 32 BK

    Baada ya hayo, Bwana akawachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawili wawili katika kila mji na kila sehemu aliyokusudia kwenda baadaye.

  21. Luka 10:2takriban 32 BK

    Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini watendakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno.

  22. Luka 10:3takriban 32 BK

    Haya! nendeni. Ninawatuma kama wana-kondoo katikati ya mbwa mwitu.

  23. Luka 10:4takriban 32 BK

    Msichukue mkoba, wala mfuko, wala viatu, na msimsalimu mtu yeyote njiani.

  24. Luka 10:5takriban 32 BK

    “Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza semeni, ‘Amani iwe kwenu.’

  25. Luka 10:6takriban 32 BK

    Kama kuna mtu wa amani humo, basi amani yenu itakuwa juu yake. La sivyo, itawarudia.