God
Mistari inayomtaja God
kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
Kwa maana njia za mtu ni wazi kabisa mbele za Bwana, naye huyapima mapito yake yote.
Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; ninachukia kiburi na majivuno, tabia mbaya na mazungumzo potovu.
“Bwana aliniumba mwanzoni mwa kazi yake, kabla ya matendo yake ya zamani;
kabla hajaumba dunia wala mashamba yake au vumbi lolote la dunia.
Nilikuwepo alipoziweka mbingu mahali pake, wakati alichora mstari wa upeo wa macho juu ya uso wa kilindi,
wakati aliweka mawingu juu na kuziweka imara chemchemi za bahari,
wakati aliiwekea bahari mpaka wake ili maji yasivunje agizo lake, na wakati aliweka misingi ya dunia.
Wakati huo nilikuwa fundi stadi kando yake. Nilijazwa na furaha siku baada ya siku, nikifurahi daima mbele zake,
nikifurahi katika dunia yake yote nami nikiwafurahia wanadamu.
Kwa maana yeyote anipataye mimi amepata uzima na kujipatia kibali kutoka kwa Bwana.
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
Yeye ambaye njia zake ni nyofu humcha Bwana, bali yeye ambaye njia zake zimepotoka humdharau Mungu.
Yeye amchaye Bwana ana ngome salama, na kwa watoto wake itakuwa kimbilio.