God
Mistari inayomtaja God
Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,
kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,
“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.
Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,
kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,
Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama, atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”
Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.