God
Mistari inayomtaja God
Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu, unayeamuru ushindi kwa Yakobo.
Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu; kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu.
bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu, unawaaibisha watesi wetu.
Katika Mungu wetu tunajivuna mchana kutwa, nasi tutalisifu jina lako milele.
Lakini sasa umetukataa na kutudhili, wala huendi tena na jeshi letu.
Umewauza watu wako kwa fedha kidogo, wala hukupata faida yoyote kwa mauzo yao.
Hayo yote yametutokea, ingawa tulikuwa hatujakusahau wala hatujaenda kinyume na agano lako.
Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma; nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako.
Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha, na ukatufunika kwa giza nene.
Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni,
je, Mungu hangaligundua hili, kwa kuwa anazijua siri za moyo?
Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.
Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? Zinduka! Usitukatae milele.
Kwa nini unauficha uso wako na kusahau taabu na mateso yetu?
Inuka na utusaidie, utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.
Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.