- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi83
Listen to this chapter
0:00
0:00
Mtunga Zaburi Aliomba Mungu Aingilie Kati
1
Wimbo. Zaburi ya Asafu. Ee Mungu, usinyamaze kimya, usinyamaze, Ee Mungu, usitulie.
2
Tazama watesi wako wanafanya fujo, jinsi adui zako wanavyoinua vichwa vyao.
Njama Dhidi ya Watu wa Mungu
3
Kwa hila, wanafanya shauri dhidi ya watu wako, wanafanya shauri baya dhidi ya wale unaowapenda.
4
Wanasema, “Njooni, tuwaangamize kama taifa, ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”
5
Kwa nia moja wanapanga mashauri mabaya pamoja, wanafanya muungano dhidi yako,
Muungano wa Mataifa ya Maadui
6
mahema ya Edomu na Waishmaeli, ya Wamoabu na Wahagari,
7
Gebali, Amoni na Amaleki, Ufilisti, pamoja na watu wa Tiro.
8
Hata Ashuru wameungana nao kuwapa nguvu wazao wa Loti.
Sala ya Hukumu kwa Kutegemea Matendo ya Zamani
9
Uwatendee kama vile ulivyowatendea Midiani, na kama vile ulivyowatendea Sisera na Yabini hapo kijito cha Kishoni,
10
ambao waliangamia huko Endori na wakawa kama takataka juu ya nchi.
11
Wafanye wakuu wao kama Orebu na Zeebu, watawala wao kama Zeba na Salmuna,
12
ambao walisema, “Na tumiliki nchi ya malisho ya Mungu.”
Lengo Kuu: Enzi Kuu ya Mungu Kufunuliwa
13
Ee Mungu wangu, wapeperushe kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi yapeperushwayo na upepo.
14
Kama vile moto uteketezavyo msitu au mwali wa moto unavyounguza milima,
15
wafuatilie kwa tufani yako na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16
Funika nyuso zao kwa aibu ili watu walitafute jina lako, Ee Bwana.
17
Wao na waaibishwe na kufadhaishwa milele, na waangamie kwa aibu.
18
Hebu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Bwana, kwamba wewe peke yako ndiwe Uliye Juu Sana ya dunia yote.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note