- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Maombolezo5
Listen to this chapter
0:00
0:00
Ombi kwa BWANA
1
Kumbuka, Ee Bwana, yaliyotupata, tazama, nawe uione aibu yetu.
2
Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni, na nyumba zetu kwa wageni.
3
Tumekuwa yatima wasio na baba, mama zetu wamekuwa kama wajane.
Uharibifu wa Kijamii na Kimwili
4
Ni lazima tununue maji tunayokunywa, kuni zetu zapatikana tu kwa kununua.
5
Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu, tumechoka na hakuna pumziko.
6
Tumejitolea kwa Misri na Ashuru tupate chakula cha kutosha.
7
Baba zetu walitenda dhambi na hawapo tena, na sisi tunachukua adhabu yao.
8
Watumwa wanatutawala na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.
9
Tunapata chakula chetu kwa kuhatarisha maisha yetu kwa sababu ya upanga jangwani.
10
Ngozi yetu ina joto kama tanuru, kwa sababu ya fadhaa itokanayo na njaa.
Kudhalilishwa na Kupoteza Heshima
11
Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni, na mabikira katika miji ya Yuda.
12
Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao, wazee hawapewi heshima.
13
Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia, wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni.
14
Wazee wameondoka langoni la mji, vijana wameacha kuimba nyimbo zao.
15
Furaha imeondoka mioyoni mwetu, kucheza kwetu kumegeuka maombolezo.
16
Taji imeanguka kutoka kichwani petu. Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi!
17
Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia, kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia,
18
kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa, nao mbweha wanatembea juu yake.
Kumwomba Mungu Anayetawala Milele
19
Wewe, Ee Bwana unatawala milele, kiti chako cha enzi chadumu kizazi hadi kizazi.
20
Kwa nini watusahau siku zote? Kwa nini umetuacha kwa muda mrefu?
21
Turudishe kwako mwenyewe, Ee Bwana, ili tupate kurudi. Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale,
22
isipokuwa uwe umetukataa kabisa na umetukasirikia pasipo kipimo.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note