Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu The Rich

145 mistari · 1 kipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.

  2. Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.

  3. Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.

  4. Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.

  5. Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”

  6. Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.

  7. Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.

  8. Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.

  9. Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.

  10. Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.

  11. Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.

  12. Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.

  13. Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!

  14. Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.

  15. Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,

  16. nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.

  17. Maskini huepukwa hata na majirani zao, bali matajiri wana marafiki wengi.

  18. Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, wanaudhania kuwa ukuta usioweza kurukwa.

  19. Mtu maskini huomba kuhurumiwa bali tajiri hujibu kwa ukali.

  20. Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.

  21. Nimeshaona uovu mzito chini ya jua: Utajiri uliolimbikizwa kwa kujinyima na kuleta madhara kwa mwenye mali,

  22. au utajiri uliopotea kwa bahati mbaya, hivyo kwamba wakati akiwa na mwana hakuna chochote kilichobaki kwa ajili yake.

  23. Zaidi ya yote, Mungu anapompa mtu yeyote utajiri na milki, humwezesha kuvifurahia, kukubali fungu lake na kuwa na furaha katika kazi yake, hii ni karama ya Mungu.

  24. Mara chache mtu huzifikiri siku za maisha yake, kwa sababu Mungu humfanya ashikwe na furaha ya moyoni.

  25. “Kwa nini niwasamehe? Watoto wenu wameniacha na kuapa kwa miungu ambayo si miungu. Niliwapatia mahitaji yao yote, lakini bado wamefanya uzinzi na kusongana katika nyumba za makahaba.