Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Friendship: General references

31 mistari · 1 kipengele

Mistari kuhusu General references

Chuja kwa kitabu
  1. Kama ndugu yako hasa, au mwanao au binti yako, au mke umpendaye, au rafiki yako wa karibu sana akikushawishi kwa siri, akisema, “Na twende tukaabudu miungu mingine” (miungu ambayo ninyi wala baba zenu hamkuifahamu,

  2. miungu ya watu wanaowazunguka, ikiwa karibu au mbali, kutoka mwisho mmoja wa nchi mpaka mwingine),

  3. usikubali wala usimsikilize. Usimhurumie! Usimwache wala usimkinge.

  4. Hakika ni lazima auawe. Ni lazima mkono wako uwe wa kwanza katika kumuua kisha mikono ya watu wengine wote.

  5. “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.

  6. Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika

  7. “Amewatenga ndugu zangu mbali nami; wale tunaojuana nao wamefarakana nami kabisa.

  8. Watu wa jamaa yangu wamekwenda mbali; rafiki zangu wamenisahau.

  9. Wageni wangu na watumishi wangu wa kike wananiona kama mgeni; wananitazama kama mgeni.

  10. Namwita mtumishi wangu, wala haitiki, ingawa namwomba kwa kinywa changu mwenyewe.

  11. Pumzi ya kinywa changu ni kinyaa kwa mke wangu; nimekuwa chukizo mno kwa ndugu zangu mwenyewe.

  12. Hata watoto wadogo hunidhihaki; ninapojitokeza, hunifanyia mzaha.

  13. Rafiki zangu wa moyoni wote wananichukia kabisa; wale niwapendao wamekuwa kinyume nami.

  14. Mimi nimebaki mifupa na ngozi tu; nimeponea nikiwa karibu kufa.

  15. “Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma, kwa kuwa mkono wa Mungu umenipiga.

  16. Kwa nini mnanifuatia kama Mungu afanyavyo? Hamtosheki kamwe na mwili wangu?

  17. Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia na nikajinyenyekesha kwa kufunga. Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,

  18. niliendelea kuomboleza kama vile wao ni rafiki au ndugu. Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni kama ninayemwombolezea mama yangu.

  19. Kama aliyenitukana ni adui yangu, ningevumilia, kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, ningejificha asinione.

  20. Kumbe ni wewe, mwenzangu, mshiriki na rafiki yangu wa karibu,

  21. ambaye awali tulifurahia ushirika mzuri, tulipokuwa tukienda na umati hekaluni mwa Mungu.

  22. Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira ya haraka, usishirikiane na yule aliye mwepesi kukasirika,

  23. la sivyo utajifunza njia zake na kujiingiza mwenyewe kwenye mtego.

  24. Usiwe mwenye kupana mikono katika rehani, au kuweka dhamana kwa ajili ya madeni.

  25. Kama ukikosa njia ya kulipa, kitanda chako kitachukuliwa ukiwa umekilalia.