Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Curse

47 mistari · 9 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Mtii Bwana Mungu wako, na kufuata amri zake na maagizo ninayokupa leo.”

  2. Siku ile ile Mose akawaagiza watu:

  3. Mtakapovuka Mto Yordani, makabila haya yatasimama juu ya Mlima Gerizimu kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benyamini.

  4. Makabila haya yatasimama juu ya Mlima Ebali kwa kutamka laana: Reubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dani na Naftali.

  5. Nao Walawi watawasomea watu wote wa Israeli kwa sauti kubwa:

  6. “Alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga au mwenye kusubu sanamu, kitu ambacho ni chukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi stadi, na kuisimamisha kwa siri.”

  7. “Alaaniwe mtu amdharauye baba yake na mama yake.”

  8. “Alaaniwe mtu asogezaye jiwe la mpaka wa jirani yake.”

  9. “Alaaniwe mtu ampotoshaye kipofu njiani.”

  10. “Alaaniwe mtu apotoshaye haki ya mgeni, yatima au mjane.”

  11. “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mke wa baba yake, kwa maana anadharau malazi ya baba yake.”

  12. “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mnyama yeyote.”

  13. “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake.”

  14. “Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mama mkwe wake.”

  15. “Alaaniwe mtu amuuaye jirani yake kwa siri.”

  16. “Alaaniwe mtu apokeaye rushwa ili kumuua mtu asiye na hatia.”

  17. “Alaaniwe mtu yule ambaye hatashikilia maneno ya sheria hii kwa kuyatekeleza.”

  18. Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali,

  19. kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.

  20. Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika.

  21. Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.

  22. Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.