Rukia maudhui

circa 1446–1406 BC

The Wilderness Years

Forty years of wandering in the desert test Israel's faith and prepare a new generation to enter the promised land.

2,247 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Kumbukumbu 10:19takriban 1491 KK

    Nanyi wapendeni wageni, kwa kuwa ninyi wenyewe mlikuwa wageni huko Misri.

  2. Kumbukumbu 10:20takriban 1491 KK

    Mche Bwana Mungu wako na umtumikie yeye. Shikamana naye kwa uthabiti na kuapa kwa jina lake.

  3. Kumbukumbu 10:21takriban 1491 KK

    Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe.

  4. Kumbukumbu 10:22takriban 1491 KK

    Baba zako walioshuka kwenda Misri jumla yao walikuwa sabini, na sasa Bwana Mungu wako amekufanya wengi kama nyota za angani.

  5. Kumbukumbu 11:1takriban 1491 KK

    Mpende Bwana Mungu wako na kushika masharti yake, amri zake, sheria zake na maagizo yake siku zote.

  6. Kumbukumbu 11:2takriban 1491 KK

    Kumbuka hivi leo kwamba sio watoto wako walioona na kujua adhabu ya Bwana Mungu wako: utukufu wake, mkono wake wenye nguvu, mkono wake ulionyooshwa;

  7. Kumbukumbu 11:3takriban 1491 KK

    ishara alizozifanya na mambo aliyoyafanya katikati ya Misri, kwa Farao mfalme wa Misri na kwa nchi yake yote;

  8. Kumbukumbu 11:4takriban 1491 KK

    lile alilolifanyia jeshi la Wamisri, farasi na magari yake, jinsi alivyowafurikisha na maji ya Bahari ya Shamu walipokuwa wakiwafuatilia ninyi, na jinsi Bwana alivyowaletea angamizo la kudumu juu yao.

  9. Kumbukumbu 11:5takriban 1491 KK

    Sio watoto wenu walioyaona yale Mungu aliyowafanyia huko jangwani mpaka mkafika mahali hapa,

  10. Kumbukumbu 11:6takriban 1491 KK

    wala lile Mungu alilowafanyia Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu wa kabila la Reubeni, wakati ardhi ilipofungua kinywa chake katikati ya Israeli yote, ikawameza pamoja na walio nyumbani mwao, hema zao na kila kitu kilichokuwa hai ambacho kilikuwa mali yao.

  11. Kumbukumbu 11:7takriban 1491 KK

    Bali ilikuwa ni macho yenu wenyewe ambayo yaliyaona mambo haya yote makuu Bwana aliyoyatenda.

  12. Kumbukumbu 11:8takriban 1491 KK

    Kwa hiyo fuateni maagizo yote ninayowapa leo, ili mpate kuwa na nguvu za kuingia na kuiteka nchi ile ambayo mnavuka Yordani kuimiliki,

  13. Kumbukumbu 11:9takriban 1491 KK

    ili mpate kuishi siku nyingi katika nchi ile ambayo Bwana aliapa kuwapa baba zenu na wazao wao, nchi itiririkayo maziwa na asali.

  14. Kumbukumbu 11:10takriban 1491 KK

    Nchi mnayoiingia kuimiliki haifanani na nchi ya Misri mlikotoka ambako mlipanda mbegu yenu na kuinywesha, kama bustani ya mboga.

  15. Kumbukumbu 11:11takriban 1491 KK

    Lakini nchi mnayovuka Yordani kuimiliki ni nchi ya milima na mabonde inywayo mvua kutoka mbinguni.

  16. Kumbukumbu 11:12takriban 1491 KK

    Ni nchi ambayo Bwana Mungu wenu anaitunza; macho ya Bwana Mungu wenu yanaitazama daima kutoka mwanzo wa mwaka hadi mwisho wa mwaka.

  17. Kumbukumbu 11:13takriban 1491 KK

    Hivyo kama mkiyatii maagizo yangu ninayowapa leo kwa uaminifu, yaani kwa kumpenda Bwana Mungu wenu, na kumtumikia kwa moyo wako wote na kwa roho yenu yote,

  18. Kumbukumbu 11:14takriban 1491 KK

    ndipo atawanyweshea mvua katika nchi yenu kwa majira yake, mvua ya masika na ya vuli, ili mpate kuvuna nafaka zenu, divai mpya na mafuta.

  19. Kumbukumbu 11:15takriban 1491 KK

    Nitawapa majani kwa ajili ya ngʼombe wenu, nanyi mtakula na kushiba.

  20. Kumbukumbu 11:16takriban 1491 KK

    Jihadharini, la sivyo mtashawishika kugeuka na kuabudu miungu mingine na kuisujudia.

  21. Kumbukumbu 11:17takriban 1491 KK

    Ndipo hasira ya Bwana itawaka dhidi yenu, naye atafunga mbingu ili mvua isinyeshe nayo ardhi haitatoa mazao, nanyi mtaangamia mara katika nchi nzuri ambayo Bwana anawapa.

  22. Kumbukumbu 11:18takriban 1491 KK

    Yawekeni haya maneno yangu katika mioyo yenu na akili zenu, yafungeni kama alama juu ya mikono yenu na kwenye paji za nyuso zenu.

  23. Kumbukumbu 11:19takriban 1491 KK

    Wafundisheni watoto wenu, yazungumzeni wakati mketipo nyumbani na wakati mtembeapo njiani, wakati mlalapo na wakati mwamkapo.

  24. Kumbukumbu 11:20takriban 1491 KK

    Yaandikeni juu ya miimo ya nyumba zenu na juu ya malango yenu,

  25. Kumbukumbu 11:21takriban 1491 KK

    ili kwamba siku zenu na siku za watoto wenu zipate kuwa nyingi katika nchi ile Bwana aliyoapa kuwapa baba zenu, kama zilivyo nyingi siku za mbingu juu ya nchi.