Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Marko 10:7takriban 29 BK

    Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’

  2. Marko 10:8takriban 29 BK

    Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.

  3. Marko 10:9takriban 29 BK

    Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”

  4. Marko 10:10takriban 29 BK

    Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili.

  5. Marko 10:11takriban 29 BK

    Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye.

  6. Marko 10:12takriban 29 BK

    Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”

  7. Marko 10:13takriban 29 BK

    Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea.

  8. Marko 10:14takriban 29 BK

    Yesu alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.

  9. Marko 10:15takriban 29 BK

    Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”

  10. Marko 10:16takriban 29 BK

    Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.

  11. Marko 10:17takriban 29 BK

    Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”

  12. Marko 10:18takriban 29 BK

    Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.

  13. Marko 10:19takriban 29 BK

    Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’ ”

  14. Marko 10:20takriban 29 BK

    Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”

  15. Marko 10:21takriban 29 BK

    Yesu akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”

  16. Marko 10:22takriban 29 BK

    Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.

  17. Marko 10:23takriban 29 BK

    Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika Ufalme wa Mungu!”

  18. Marko 10:24takriban 29 BK

    Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika Ufalme wa Mungu.

  19. Marko 10:25takriban 29 BK

    Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajirikuingia katika Ufalme wa Mungu.”

  20. Marko 10:26takriban 29 BK

    Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”

  21. Marko 10:27takriban 29 BK

    Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”

  22. Marko 10:28takriban 29 BK

    Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”

  23. Marko 10:29takriban 29 BK

    Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili,

  24. Marko 10:30takriban 29 BK

    ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao.

  25. Marko 10:31takriban 29 BK

    Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”