- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi73
Listen to this chapter
0:00
0:00
Mapambano ya Kwanza ya Mtunga Zaburi
1
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
Ufanisi wa Udanganyifu wa Waovu
4
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
Shaka na Kukata Tamaa
13
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
Mabadiliko Katika Patakatifu
17
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Mungu Ndiye Nguvu ya Moyo Wangu
21
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
Uhakika na Tumaini la Milele
23
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note