Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu The Poor: Oppress

8 mistari · 92 vipengele

Mistari kuhusu Oppress

  1. Humsukuma mhitaji kutoka njia, na kuwafanya maskini wote wa nchi kulazimika kujificha.

  2. Kama punda-mwitu jangwani, maskini huzunguka katika kazi zao za kutafuta chakula; mahali palipo jangwa huwapa chakula cha watoto wao.

  3. Hukusanya chakula mashambani na kuokota masazo katika mashamba ya mizabibu ya waovu.

  4. Kwa kukosa nguo, usiku kucha hukaa uchi; hawana chochote cha kujifunika baridi.

  5. Hutota kwa mvua za mlimani, nao huikumbatia miamba kwa ajili ya kukosa pa kujisitiri.

  6. Mtoto yatima hupokonywa matitini; mtoto wachanga wa maskini hunyakuliwa kwa ajili ya deni.

  7. Kwa kukosa nguo, hutembea uchi; hubeba miganda ya ngano, lakini huwa na njaa.

  8. Huwaonea maskini na wahitaji. Hunyangʼanyana. Harudishi kile kilichowekwa rehani kwake. Huziinulia sanamu macho. Hufanya mambo ya machukizo.