Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Privileges of Saints

91 mistari · 36 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Waovu watakaposogea dhidi yangu ili wanile nyama yangu, adui zangu na watesi wangu watakaponishambulia, watajikwaa na kuanguka.

  2. Hata jeshi linizunguke pande zote, moyo wangu hautaogopa; hata vita vitokee dhidi yangu, hata hapo nitakuwa na ujasiri.

  3. Jambo moja ninamwomba Bwana, hili ndilo ninalolitafuta: niweze kukaa nyumbani mwa Bwana siku zote za maisha yangu, niutazame uzuri wa Bwana na kumtafuta hekaluni mwake.

  4. Kwa kuwa siku ya shida, atanihifadhi salama katika maskani yake, atanificha uvulini mwa hema yake na kuniweka juu kwenye mwamba.

  5. Ninaikabidhi roho yangu mikononi mwako, unikomboe Ee Bwana, uliye Mungu wa kweli.

  6. Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.

  7. Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu, unayeamuru ushindi kwa Yakobo.

  8. Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.

  9. Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

  10. Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.

  11. na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”

  12. Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu, ngome imara dhidi ya adui.

  13. Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.

  14. Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.

  15. Maombi ya Mose, mtu wa Mungu. Bwana, wewe umekuwa makao yetu katika vizazi vyote.

  16. Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,

  17. wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.

  18. Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.

  19. Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.

  20. Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,

  21. basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.

  22. Kabla sijapata shida nilipotea njia, lakini sasa ninalitii neno lako.

  23. hakika, yeye alindaye Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi.

  24. Bwana anakulinda, Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,

  25. Hakika Mungu ni wokovu wangu; nitamtumaini wala sitaogopa. Bwana, Bwana, ni nguvu zangu na wimbo wangu; amekuwa wokovu wangu.”