Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Persecution: Of Jesus

152 mistari · 61 vipengele

Mistari kuhusu Of Jesus

Chuja kwa kitabu
  1. Nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na wake, yeye atakuponda kichwa, nawe utamuuma kisigino.”

  2. Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?

  3. Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.

  4. Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”

  5. Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.

  6. Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,

  7. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?

  8. Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.

  9. Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.

  10. Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:

  11. Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”

  12. Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.

  13. Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.

  14. Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.

  15. Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.

  16. Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.

  17. Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.

  18. Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.

  19. Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.

  20. Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.

  21. Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.

  22. Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.

  23. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi.” Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, niokoe, kwa maana maji yamenifika shingoni.

  24. Ninazama kwenye vilindi vya matope, pasipo mahali pa kukanyaga, Nimefika kwenye maji makuu, mafuriko yamenigharikisha.

  25. Nimechoka kwa kuomba msaada, koo langu limekauka. Macho yangu yanafifia, nikimtafuta Mungu wangu.