Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Gospel

110 mistari · 2 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.

  2. Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.

  3. “Siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.

  4. Halitafanana na agano nililofanya na baba zao wakati nilipowashika mkono kuwaongoza watoke Misri, kwa sababu walivunja agano langu, ijapokuwa nilikuwa mume kwao,” asema Bwana.

  5. “Hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli baada ya siku zile,” asema Bwana. “Nitaweka sheria yangu katika nia zao, na kuiandika mioyoni mwao. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

  6. Mtu hatamfundisha tena jirani yake, wala mtu kumfundisha ndugu yake akisema, ‘Mjue Bwana Mungu,’ kwa sababu wote watanijua mimi, tangu aliye mdogo kabisa kwao, hadi aliye mkuu sana,” asema Bwana. “Kwa sababu nitasamehe uovu wao, wala sitazikumbuka dhambi zao tena.”

  7. Yesu akajibu, “Rudini mkamwambie Yohana yale mnayosikia na kuyaona:

  8. Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.

  9. Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”

  10. Yesu akawajia na kusema, “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.

  11. Kwa sababu hii, enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu,

  12. nanyi wafundisheni kuyashika mambo yote niliyowaamuru ninyi. Hakika mimi niko pamoja nanyi siku zote, hadi mwisho wa nyakati.”

  13. Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,

  14. akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”

  15. Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:

  16. “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.

  17. Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,

  18. kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani,

  19. kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:

  20. ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,

  21. kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:

  22. kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu

  23. katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.

  24. “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,

  25. kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,