- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Adultery: General references
Mistari kuhusu General references
Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto wakati wa usiku na kumwambia, “Wewe ni kama mfu kwa sababu ya huyu mwanamke uliyemchukua; yeye ni mke wa mtu.”
Lakini kwa sababu kwa kufanya hili umefanya adui za Bwana kuonyesha dharau kabisa, mwana atakayezaliwa kwako atakufa.”
Jicho la mzinzi hungojea wakati wa giza, naye hufikiri, ‘Hakuna jicho litakaloniona,’ naye huuficha uso wake.
Katika giza, huvunja majumba, lakini wakati wa mchana hujifungia ndani; hawataki kufanya lolote nuruni.
Kwa wote hawa, giza nene ndiyo asubuhi yao; hujifanya rafiki na vitisho vya gizani.
“Lakini wao ni povu juu ya maji; sehemu yao juu ya nchi imelaaniwa, hivyo hakuna hata mmoja aendaye kwenye shamba la mizabibu.
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba hudondoza asali, na maneno ya kinywa chake ni laini kuliko mafuta;
lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo, mkali kama upanga ukatao kuwili.
Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo; hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini.
Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima; njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.
Sasa basi wanangu, nisikilizeni; msiache ninalowaambia.
Njia zenu ziwe mbali naye, msiende karibu na mlango wa nyumba yake,
usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine na miaka yako kwa aliye mkatili,
wageni wasije wakasherehekea utajiri wako na jitihada yako ikatajirisha nyumba ya mwanaume mwingine.
Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu, wakati nyama na mwili wako vimechakaa.
Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu! Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!