Rukia maudhui

circa 1446–1406 BC

The Wilderness Years

Forty years of wandering in the desert test Israel's faith and prepare a new generation to enter the promised land.

2,247 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Kumbukumbu 14:15takriban 1451 KK

    mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,

  2. Kumbukumbu 14:16takriban 1451 KK

    bundi, mumbi, bundi mkubwa,

  3. Kumbukumbu 14:17takriban 1451 KK

    mwari, nderi, mnandi,

  4. Kumbukumbu 14:18takriban 1451 KK

    korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.

  5. Kumbukumbu 14:19takriban 1451 KK

    Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.

  6. Kumbukumbu 14:20takriban 1451 KK

    Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.

  7. Kumbukumbu 14:21takriban 1451 KK

    Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.

  8. Kumbukumbu 14:22takriban 1451 KK

    Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka.

  9. Kumbukumbu 14:23takriban 1451 KK

    Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima.

  10. Kumbukumbu 14:24takriban 1451 KK

    Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana),

  11. Kumbukumbu 14:25takriban 1451 KK

    basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua.

  12. Kumbukumbu 14:26takriban 1451 KK

    Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi.

  13. Kumbukumbu 14:27takriban 1451 KK

    Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.

  14. Kumbukumbu 14:28takriban 1451 KK

    Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu,

  15. Kumbukumbu 14:29takriban 1451 KK

    ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.

  16. Kumbukumbu 15:1takriban 1451 KK

    Kila mwisho wa miaka saba ni lazima mfute madeni.

  17. Kumbukumbu 15:2takriban 1451 KK

    Hivi ndivyo itakavyofanyika: Kila mkopeshaji atafuta mkopo aliomkopesha Mwisraeli mwenzake. Hatamtaka Mwisraeli mwenzake au ndugu yake amlipe hilo deni, kwa sababu wakati wa Bwana wa kufuta madeni umetangazwa.

  18. Kumbukumbu 15:3takriban 1451 KK

    Unaweza kudai malipo kwa mgeni, lakini lazima ufute kila deni ambalo unamdai ndugu yako.

  19. Kumbukumbu 15:4takriban 1451 KK

    Hata hivyo, hapatakuwepo maskini miongoni mwenu, kwa kuwa katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kuimiliki kama urithi wenu, atawabariki sana,

  20. Kumbukumbu 15:5takriban 1451 KK

    ikiwa tutamtii Bwana Mungu wenu kikamilifu na kuwa waangalifu kuyafuata maagizo haya yote ninayowapa leo.

  21. Kumbukumbu 15:6takriban 1451 KK

    Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki kama alivyoahidi, nanyi mtawakopesha mataifa mengi lakini hamtakopa kwa yeyote. Mtatawala mataifa mengi lakini hakuna taifa litakalowatawala ninyi.

  22. Kumbukumbu 15:7takriban 1451 KK

    Ikiwa kuna mtu maskini miongoni mwa ndugu zenu, katika mji wowote wa hiyo nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msiwe na moyo mgumu wala usimfumbie mkono ndugu yako aliye maskini.

  23. Kumbukumbu 15:8takriban 1451 KK

    Afadhali fungua mikono yako na umkopeshe kwa hiari chochote anachohitaji.

  24. Kumbukumbu 15:9takriban 1451 KK

    Jihadhari usijiwekee wazo hili ovu: “Mwaka wa saba, mwaka wa kufuta madeni umekaribia,” usije ukaonyesha nia mbaya kwa ndugu yako mhitaji na ukaacha kumpa chochote. Anaweza kumlalamikia Bwana dhidi yako nawe utakuwa umepatikana na hatia ya dhambi.

  25. Kumbukumbu 15:10takriban 1451 KK

    Mpe kwa ukarimu na ufanye hivyo bila kinyongo moyoni, ndipo kwa sababu ya hili Bwana Mungu wenu atakubariki katika kazi zako zote na kwa kila kitu utakachokiwekea mkono wako.