Rukia maudhui

circa 1446–1406 BC

The Wilderness Years

Forty years of wandering in the desert test Israel's faith and prepare a new generation to enter the promised land.

2,247 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Hesabu 27:1takriban 1452 KK

    Binti za Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, walikuwa wa koo za Manase mwana wa Yosefu. Majina ya hao binti yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa. Walikaribia

  2. Hesabu 27:2takriban 1452 KK

    ingilio la Hema la Kukutania na kusimama mbele ya Mose, kuhani Eleazari, viongozi na kusanyiko lote, wakasema,

  3. Hesabu 27:3takriban 1452 KK

    “Baba yetu alikufa jangwani. Hakuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora, ambao walifungamana pamoja dhidi ya Bwana, lakini alikufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe na hakuacha wana.

  4. Hesabu 27:4takriban 1452 KK

    Kwa nini jina la baba yetu lifutike kutoka ukoo wake kwa sababu hakuwa na mwana? Tupatie milki miongoni mwa ndugu za baba yetu.”

  5. Hesabu 27:5takriban 1452 KK

    Kwa hiyo Mose akalileta shauri lao mbele za Bwana,

  6. Hesabu 27:6takriban 1452 KK

    naye Bwana akamwambia Mose,

  7. Hesabu 27:7takriban 1452 KK

    “Wanachosema binti za Selofehadi ni sawa. Ni lazima kwa hakika uwape milki kama urithi miongoni mwa ndugu za baba yao, na kubadili urithi wa baba yao uwe wao.

  8. Hesabu 27:8takriban 1452 KK

    “Waambie Waisraeli, ‘Ikiwa mtu atakufa naye hakuacha mwana, utampa binti yake urithi wake.

  9. Hesabu 27:9takriban 1452 KK

    Ikiwa hana binti, wape ndugu zake wa kiume urithi wake.

  10. Hesabu 27:10takriban 1452 KK

    Ikiwa hana ndugu wa kiume toa urithi wake kwa ndugu za baba yake.

  11. Hesabu 27:11takriban 1452 KK

    Ikiwa baba yake hakuwa na ndugu wa kiume, toa urithi wake kwa ndugu wa karibu katika ukoo wake, ili aumiliki. Hili litakuwa dai la sheria kwa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru Mose.’ ”

  12. Hesabu 27:12takriban 1452 KK

    Kisha Bwana akamwambia Mose, “Panda juu ya mlima huu katika kilele cha Abarimu uione nchi ambayo nimewapa Waisraeli.

  13. Hesabu 27:13takriban 1452 KK

    Baada ya kuiona, wewe pia utakusanywa pamoja na watu wako kama ndugu yako Aroni alivyokusanywa,

  14. Hesabu 27:14takriban 1452 KK

    kwa kuwa jumuiya ilipoasi amri yangu kwenye maji katika Jangwa la Sini, wakati jumuiya ilipogombana nami, nyote wawili mliacha kuitii amri yangu ya kuniheshimu kama mtakatifu mbele ya macho yao.” (Haya yalikuwa maji ya Meriba huko Kadeshi, katika Jangwa la Sini.)

  15. Hesabu 27:15takriban 1452 KK

    Mose akamwambia Bwana,

  16. Hesabu 27:16takriban 1452 KK

    “Bwana, Mungu wa roho zote za wanadamu, na amteue mtu juu ya jumuiya hii

  17. Hesabu 27:17takriban 1452 KK

    ili atoke na kuingia mbele yao, atakayewaongoza katika kutoka kwao na kuingia kwao, ili watu wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”

  18. Hesabu 27:18takriban 1452 KK

    Kwa hiyo Bwana akamwambia Mose, “Mchukue Yoshua mwana wa Nuni, mtu ambaye Roho yuko ndani yake, uweke mkono juu yake.

  19. Hesabu 27:19takriban 1452 KK

    Msimamishe mbele ya kuhani Eleazari pamoja na kusanyiko lote, umpe maagizo mbele yao.

  20. Hesabu 27:20takriban 1452 KK

    Mpe sehemu ya mamlaka yako ili jumuiya yote ya Waisraeli ipate kumtii.

  21. Hesabu 27:21takriban 1452 KK

    Atasimama mbele ya kuhani Eleazari, ambaye atapokea maamuzi kwa ajili yake, kwa kuuliza mbele za Bwana kwa ile Urimu. Kwa amri yake, yeye na jumuiya yote ya Waisraeli watatoka, na kwa amri yake, wataingia.”

  22. Hesabu 27:22takriban 1452 KK

    Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza. Akamtwaa Yoshua na kumsimamisha mbele ya kuhani Eleazari na kusanyiko lote.

  23. Hesabu 27:23takriban 1452 KK

    Kisha akaweka mikono yake juu ya kichwa cha Yoshua na kumpa maagizo, kama vile Bwana alivyoelekeza kupitia kwa Mose.

  24. Hesabu 28:1takriban 1452 KK

    Bwana akamwambia Mose,

  25. Hesabu 28:2takriban 1452 KK

    “Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’