Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 13:2takriban 33 BK

    Yesu akawauliza, “Mnadhani kwamba hawa Wagalilaya ambao walikufa kifo cha namna hiyo walikuwa na dhambi kuwazidi Wagalilaya wengine wote?

  2. Luka 13:3takriban 33 BK

    La hasha! Ninyi nanyi msipotubu, mtaangamia vivyo hivyo.

  3. Luka 13:4takriban 33 BK

    Au wale watu kumi na wanane waliokufa walipoangukiwa na mnara huko Siloamu: mnadhani wao walikuwa waovu kuliko watu wote waliokuwa wanaishi Yerusalemu?

  4. Luka 13:5takriban 33 BK

    Nawaambia, la hasha! Ninyi nanyi msipotubu, wote mtaangamia vivyo hivyo.”

  5. Luka 13:6takriban 33 BK

    Kisha Yesu akawaambia mfano huu: “Mtu mmoja alikuwa na mtini uliopandwa katika shamba lake la mizabibu, akaja ili kutafuta tini kwenye mti huo, lakini hakupata hata moja.

  6. Luka 13:7takriban 33 BK

    Hivyo akamwambia mtunza shamba: ‘Tazama, kwa muda wa miaka mitatu sasa nimekuwa nikija kutafuta matunda kwenye mtini huu, nami sikupata hata moja. Ukate! Kwa nini uendelee kuharibu ardhi?’

  7. Luka 13:8takriban 33 BK

    “Yule mtunza shamba akamjibu, ‘Bwana, uache tena kwa mwaka mmoja zaidi, nami nitaupalilia na kuuwekea mbolea.

  8. Luka 13:9takriban 33 BK

    Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vyema, la sivyo uukate.’ ”

  9. Luka 13:10takriban 33 BK

    Basi Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo siku ya Sabato.

  10. Luka 13:11takriban 33 BK

    Wakati huo huo akaja mwanamke mmoja aliyekuwa na pepo mchafu, naye alikuwa amepinda mgongo kwa muda wa miaka kumi na minane, wala alikuwa hawezi kunyooka wima.

  11. Luka 13:12takriban 33 BK

    Yesu alipomwona, akamwita, akamwambia, “Mwanamke, uwe huru, umepona ugonjwa wako.”

  12. Luka 13:13takriban 33 BK

    Yesu alipomwekea mikono yake, mara akasimama wima akaanza kumtukuza Mungu.

  13. Luka 13:14takriban 33 BK

    Lakini kiongozi wa sinagogi akakasirika kwa sababu Yesu alikuwa ameponya mtu siku ya Sabato. Akaambia ule umati wa watu, “Kuna siku sita ambazo watu wanapaswa kufanya kazi. Katika siku hizo, njooni mponywe, lakini si katika siku ya Sabato.”

  14. Luka 13:15takriban 33 BK

    Lakini Bwana akamjibu, “Enyi wanafiki! Je, kila mmoja wenu hamfungulii ngʼombe wake au punda wake kutoka zizini akampeleka kumnywesha maji siku ya Sabato?

  15. Luka 13:16takriban 33 BK

    Je, huyu mwanamke, ambaye ni binti wa Abrahamu, aliyeteswa na Shetani akiwa amemfunga kwa miaka yote hii kumi na minane, hakustahili kufunguliwa kutoka kifungo hicho siku ya Sabato?”

  16. Luka 13:17takriban 33 BK

    Aliposema haya, wapinzani wake wakaaibika, lakini watu wakafurahi kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyoyafanya.

  17. Luka 13:18takriban 33 BK

    Kisha Yesu akauliza, “Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaufananisha na nini?

  18. Luka 13:19takriban 33 BK

    Umefanana na punje ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake. Nayo ikakua, ikawa mti nao ndege wa angani wakatengeneza viota vyao kwenye matawi yake.”

  19. Luka 13:20takriban 33 BK

    Yesu akauliza tena, “Nitaufananisha Ufalme wa Mungu na nini?

  20. Luka 13:21takriban 33 BK

    Unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”

  21. Luka 13:22takriban 33 BK

    Yesu akapita katika miji na vijiji, akifundisha wakati alisafiri kwenda Yerusalemu.

  22. Luka 13:23takriban 33 BK

    Mtu mmoja akamuuliza, “Bwana, ni watu wachache tu watakaookolewa?”

  23. Luka 13:24takriban 33 BK

    Yesu akawaambia, “Jitahidini sana kuingia kupitia mlango mwembamba, kwa maana nawaambia wengi watajaribu kuingia, lakini hawataweza.

  24. Luka 13:25takriban 33 BK

    Wakati mwenye nyumba atakapoondoka na kufunga mlango, mtasimama nje mkibisha mlango na kusema, ‘Bwana! Tufungulie mlango!’ “Lakini yeye atawajibu, ‘Siwajui ninyi, wala mtokako.’

  25. Luka 13:26takriban 33 BK

    “Ndipo mtamjibu, ‘Tulikula na kunywa pamoja nawe, tena ulifundisha katika mitaa yetu.’